-
Sababu za Ripota wa UN za kuonya kuhusu kuendelea Ulaya kuipa silaha Israel
Nov 21, 2025 22:54Umoja wa Mataifa umeonya kuhusu kuendelea nchi za Ulaya kuisheheneza silaha Israel licha ya kwamba kuna ushahidi wa kutosha na usiopingika wa jinsi utawala wa Kizayuni unavyotumia silaha hizo kufanya jinai na mauaji ya umati dhidi ya watu wasio na hatia.
-
Israel yafanya mashambulio ya kinyama Ghaza, yaua Wapalestina 28 na kujeruhi 77
Nov 20, 2025 02:39Wapalestina wasiopunguua 28 wameuawa shahidi katika wimbi jipya la mashambulizi ya kinyama yanayofanywa na jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel kwenye Ukanda wa Ghaza, yakiwa ni moja ya ukiukaji mkubwa zaidi wa makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyosimamiwa na Marekani na kuanza kutekelezwa mwezi uliopita wa Oktoba.
-
'Siku ya fedheha’: Afisa wa zamani wa haki za binadamu wa UN akosoa azimio la UNSC kuhusu Gaza
Nov 19, 2025 03:26Afisa wa ngazi ya juu wa zamani wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa amelaani hatua ya Baraza la Usalama la umoja huo ya kupitishaa azimio linalounga mkono mpango wa Marekani wa kuanzisha kikosi cha kimataifa cha kurejesha utulivu katika Ukanda wa Gaza uliozingirwa, akiitaja kura hiyo kuwa ni "siku ya fedheha" kwa chombo hicho cha dunia.
-
Jihadul-Islami: Muqawama hautaitambua Israel, hakutakuwa na suluhu bila Palestina kupata haki zake
Nov 15, 2025 22:59Mwakilishi wa harakati ya Jihadul-Islami ya Palestina hapa mjini Tehran amesema: "sisi katika mavuguvugu ya Muqawama wa Kiislamu hatutambui uwepo wa utawala wa Kizayuni na hatulazimiki kuutambua, hasa kwa vile utawala huu hautambui hata uwepo wa watu wa Palestina."
-
Kwa nini China na Russia zimepinga azimio lililopendekezwa na Marekani kuhusu Gaza?
Nov 15, 2025 22:56Russia na China ambazo ni wanachama wa kudumu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa zimetaka kufutwa kikamilifu "Tume ya Amani" kwenye matini ya rasimu iliyowasilishwa na Marekani kwenye baraza kuhusu Gaza.
-
Maiti zingine 51 za Wapalestina waliouliwa shahidi na jeshi la kizayuni zagunduliwa Ghaza
Nov 14, 2025 04:13Timu za uokoaji za Palestina katika Ukanda wa Ghaza zimegundua na kufukua maiti zingine 51 za Wapalestina waliouliwa shahidi na jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel.
-
Maafa ya vita vya kinyama vya Israel yamepelekea Wapalestina 6,000 wa Ghaza kukatwa viungo
Nov 13, 2025 23:07Wizara ya Afya ya Palestina katika Ukanda wa Ghaza imetoa ripoti inayoonyesha kuwa, Wapalestina 6,000 wamekatwa viungo katika eneo hilo tangu utawala wa kizayuni wa Israael ulipoanzisha vita vya kinyama Oktoba 2023 ambavyo vimeendelea kwa muda wa miaka miwili.
-
HAMAS: Silaha za Muqawama haziwezi kujadiliwa kabla ya kuundwa kwanza nchi ya Palestina
Nov 12, 2025 08:40Osama Hamdan, kiongozi mwandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS, amesisitiza kwamba, silaha za Muqawama ni suala lisiloweza kujadiliwa kabla ya kuundwa nchi dola ya Palestina na akabainisha kuwa, lengo la kisiasa la Muqawama litabaki kuwa ni kuikomboa ardhi, kuundwa nchi huru ya Palestina ambayo mji mkuu wake ni Baitul-Muqaddas na kuwepo hakikisho la kurejea wakimbizi.
-
WHO: Zaidi ya wagonjwa 16,000 huko Gaza wanasubiri kupelekwa nje kwa ajili ya matibabu
Nov 11, 2025 07:15Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema kuwa wagonjwa wasiopungua 16,500 katika Ukanda wa Gaza wanasubiri kupelekwa nje kwa ajili ya matibabu na kusisitiza kuwa suhula zake za tiba ziko tayari mpakani lakini haziwezi kuingia katika eneo hilo kufuatia Israel kufunga vivuko hivyo.
-
HAMAS: Lengo la safari ya rais wa Israel Afrika ni kubadilisha misimamo ya nchi zinazounga mkono Palestina
Nov 10, 2025 02:48Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imetangaza kuwa safari ya rais wa utawala ghasibu wa kizayuni katika nchi za Afrika ni jaribio la kutaka kubadilisha msimamo wa nchi hizo wa zinazopinga ukoloni na kuunga mkono haki za watu wa Palestina.