-
Hamas: Nchi zinazounga mkono mashambulizi ya Israel zinahusika katika mauaji ya watoto na wanawake
Oct 17, 2023 00:17Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) ilisema jana Jumatatu kuwa, nchi zinazounga mkono uvamizi wa Israel katika hujuma yake inayoendelea dhidi ya Ukanda wa Gaza unaozingirwa zinahusika katika mauaji ya watoto, wanawake na raia.
-
Velayati: Kusimama kidete muqawama ndio njia sahihi ya kufikia kilele cha ushindi
Oct 16, 2023 10:16Mshauri wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu katika masuala ya kimataifa amesema kuwa, kusimama kidete muqawama ndio njia sahihi ya kufikia kilele cha ushindi.
-
Raisi: Inapasa kuwabebesha dhima wanaonyamazia kimya jinai za Israel
Oct 15, 2023 23:38Rais Ebrahim Raisi wa Iran amesema kuliunga mkono taifa linalodhulumiwa la Palestina ni katika misingi ya sera za Jamhuri ya Kiislamu na kuongeza kuwa, wanaonyamazia kimya jinai za Israel watabeba mas'ulia mbele ya Mwenyezi Mungu, mienendo yao na historia.
-
Ni mbwa, si mtoto.. Mwandishi habari wa Marekani afichua uongo wa Netanyahu, madai ya Hamas kuua watoto
Oct 15, 2023 22:59Mwandishi wa habari wa Marekani, Jackson Hinkle, meifichua uwongo wa picha iliyodaiwa ni ya mtoto aliyeungua moto iliyochapishwa na Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, aliyesema kwamba ilikuwa ya mtoto wa Kiisraeli aliyechomwa moto na wapiganaji wa Harakati ya mapambano ya Kislamu ya Palestina (Hamas).
-
Wakenya wawasha mishumaa kuonyesha mshikamano na Wapalestina
Oct 15, 2023 07:58Wananchi wa Kenya wamekusanyika na kuwawasha mishumaa katika mji mkuu wa nchi hiyo, Nairobi kuonyesha mshikamano wao na wananchi wa Palestina. Mashirika yaliyoandaa shughuli hiyo ni pamoja na Kenyans 4 Palestine, The Pan African Palestine Solidarity Network (PAPSN) na podkasti ya 'Until Everyone is Free.'
-
Sisitizo la Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu la kuungwa mkono Wapalestina
Oct 15, 2023 04:11Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, jana (Jumamosi) alionana na Sheikh Ibrahim Zakzaky, Mkuu wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria na familia yake hapa mjini Tehran na sambamba na kugusia hali ya ardhi za Palestina hivi sasa hasa Ghaza amesema, leo hii moja ya madhihirisho ya nguvu za Uislamu ni haya mambo yanayotokea hivi sasa huko Palestina.
-
Maandamano ya kuwaunga mkono Wapalestina yafanyika tena Afrika Kusini
Oct 14, 2023 03:54Kwa mara nyingine, wananchi wa Afrika Kusini wamefanya maandamano wakionyesha mshikamano wao na watu wanaodhulumiwa wa Palestina na kutangaza uungaji mkono wao kwa mapambano ya ukombozi wa Palestina.
-
Iran yakosoa taarifa ya Arab League kuhusu Gaza
Oct 14, 2023 03:32Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema taarifa mpya ya Jumuiya ya Nchi za Kiarabu juu ya matukio ya Ukanda wa Gaza inakera na kufedhehesha.
-
Khatibu wa Swala ya Ijumaa Tehran: Kuongezeka Waislamu wanaounga mkono muqawama wa Palestina ni dhihirisho la Mwamko wa Kiislamu
Oct 13, 2023 08:41Khatibu wa Swala ya Ijumaa katika mji wa Tehran amesema kuwa kujitokeza wimbi kubwa na uungaji mkono wa Waislamu katika maeneo mbalimbali duniani kwa mapambano ya wananchi wa Palestina ni jambo lenye baraka na la kusifiwa linalodhihirisha mwamko wa Kiislamu.
-
Maelfu ya Watunisia waandamana kuwaunga mkono Wapalestina
Oct 13, 2023 03:43Maelfu ya wananchi wa Tunisia wamefanya maandamano wakionyesha mshikamano wao na wananchi wanaodhulumiwa wa Palestina sanjari na kulaani jinai zinazofanywa na utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina.