-
HAMAS: Mielekeo ya Mamlaka ya Ndani ipo dhidi ya taifa la Palestina
Feb 21, 2023 03:54Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imesema mapatano yaliyofikiwa karibuni baina ya Mamlaka ya Ndani ya Palestina na utawala haramu wa Israel kwa mashinikizo ya Marekani ni usaliti kwa kambi ya muqawama ya Wapalestina.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran atoa pole ya kifo cha balozi mkongwe wa Palestina
Feb 20, 2023 23:02Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ametoa mkono wa pole kufuatia kifo cha balozi wa miaka mingi na mkongwe wa Palestina, hapa nchini Iran. Balozi Salah al Zawawi alifariki dunia jana Jumatatu akiwa na umri wa miaka 85 katika hospitali moja ya hapa mjini Tehran.
-
Kiongozi Muadhamu azikosoa nchi za Waislamu kwa kufumbia macho kadhia ya Palestina
Feb 18, 2023 07:28Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amezikosoa nchi za Kiislamu kwa kutochokua hatua yoyote ya maana juu ya kadhia ya Palestina.
-
Nchi za Amerika ya Latini zalaani ujenzi wa vitongoji haramu
Feb 18, 2023 06:23Kundi la nchi za Amerika ya Latini limelaani na kukosoa vikali uamuzi wa serikali ya Israel yenye misimamo ya kufurutu ada ya Benjamin Netanyahu wa kuidhinisha ujenzi wa vitongoji vipya tisa katika ardhi za Wapalestina za Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Al-Nakhalah ampongeza Kiongozi wa Mapinduzi kwa mnasaba wa ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran
Feb 12, 2023 08:25Katibu Mkuu wa Harakati ya Jihad Iislami ya Palestina, Ziyad al-Nakhalah amemtumia ujumbe Kiongozi Muadhamu wa Mapiinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Ali Khamenei akimpongeza kwa mnasaba wa kutimia miaka 44 ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran.
-
UN: Israel imeua makumi ya Wapalestina ndani ya wiki tatu
Feb 05, 2023 07:13Vikosi vya utawala haramu wa Israel vimewaua shahidi makumi ya Wapalestina katika kipindi cha wiki tatu, katika eneo la Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan linalokaliwa kwa mabavu, hayo yamesemwa na Umoja wa Mataifa.
-
Iran: Wakiukaji wa kila siku wa haki za binadamu ni wabeba bendera ya uongo ya haki za binadamu
Feb 04, 2023 07:15Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, watu ambao ndio wakiukaji wakubwa wa kila siku wa haki za binadamu ulimwenguni, leo ni wabeba bendera ya uongo ya kutetea haki za binadamu.
-
Wanamuqawama wa Palestina wajibu mashambulizi ya anga ya utawala wa Kizayuni Ghaza
Feb 02, 2023 04:37Utawala wa Kizayuni leo asubuhi umeyashambulia maeneo kadhaa katika Ukanda wa Ghaza ambapo hujuma hiyo imekabiliwa na jibu la makundi ya wanamuqawama wa Palestina ambao wamevurumisha maroketi kadhaa katika vitongoji vya walowezi wa Kizayuni kandokando ya Ukanda wa Ghaza.
-
Nyaraka za Uingereza: Bush aliiamuru CIA kutafuta shakhsia mbadala wa Arafat
Feb 02, 2023 04:24Rais wa zamani wa Marekani George W Bush aliliamuru Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA) kumtafuta shakhsia mbadala ili kuchukua nafasi ya aliyekuwa Kiongozi wa Palestina mwendazake Yasser Arafat baada ya kupamba moto Intifadha ya Pili ya Wapalestina mwaka 2001. Hayo ni kwa mujibu wa nyaraka za Uingereza zilizotolewa hadharani.
-
Algeria: Palestina itaendelea kuwa kadhia kuu ya Ulimwengu wa Kiislamu
Jan 30, 2023 03:26Rais wa Algeria amesema kukwa, Palestina itaendelea kuwa kadhiaa kuu ya Ulimwengu wa Kiislamu na Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC.