-
Qatar yapinga hatua za Saudi Arabia huko Yemen
Jun 22, 2018 03:16Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar amesema kuwa nchi yake inapinga hatua za muungano vamizi wa Saudi Arabia huko Yemen.
-
Rais Rouhani: Iran itaendelea kuwa pamoja na Qatar
Jun 18, 2018 10:55Rais Hassan Rouhani amekaribisha kustawishwa uhusiano wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Qatar na kusisitiza kuwa hakuna kizuizi chochote cha kuzuia kustawishwa uhusiano huo na kwamba Tehran itaendelea kuwa pamoja na Doha.
-
Qatar yamteua balozi mpya maalumu kuhudumu Iran
Jun 14, 2018 03:18Sheikh Tamim bin Hamad, Amiri wa Qatar, amemteua Mohammed bin Hamad Al Hajri kuwa balozi mpya maalumu wa nchi hiyo katika Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Qatar yaishtaki Imarati katika mahakama ya haki za binadamu ya UN
Jun 12, 2018 09:20Qatar imewasilisha faili la kesi dhidi ya Umoja wa Falme za Kiarabu, katika mahakama ya juu zaidi ya Umoja wa Mataifa, ikiituhumu Abu Dhabi kwamba imekiuka haki za binadamu za wananchi wa Qatar, huku mgogoro wa nchi hizo za Kiarabu ukielekea kutimiza mwaka mmoja.
-
Kiongozi wa HAMAS: Iran ni nchi muhimu na mhimili wa msingi katika eneo
Jun 11, 2018 10:30Mkuu wa ofisi ya kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina (HAMAS) ameuenzi na kuusifu mchango wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika kuihami na kuiunga mkono Palestina na kusisitiza kwamba: Hamas haiungi mkono mhimili wowote wa Kiarabu au wa kieneo dhidi ya mhimili mwengine.
-
Qatar: Saudia iache kuingiza masuala ya dini katika mgogoro wa kisiasa
Jun 06, 2018 09:50Wizara ya Wakfu na Masuala ya Kiislamu nchini Qatar sambamba na kuelezea mwenendo wa vizuizi vinavyofanywa na Saudia kwa ajili ya kuwazuia raia wa nchi hiyo kuweza kushiriki ibada ya hija, imeitaka Riyadh kuacha kuyaingiza masuala ya kidini katika mgogoro wa kisiasa wa pande mbili.
-
Mwaka mmoja wa mgogoro kati ya nchi za Kiarabu
Jun 06, 2018 01:27Umetimia mwaka mmoja tokea uanze mgogoro baina ya nchi za Kiarabu na dalili zote zinaonyesha kuwa mgogoro huo ungali unaendelea bali hata utazidi kupanuka na kuwa mbaya zaidi.
-
Qatar: Mliotuwekea vikwazo acheni ndoto za alinacha
Jun 05, 2018 09:33Katika hali inayoonekana ni ya kutoweka matumaini ya kutatuliwa hivi karibuni mgogoro wa Qatar na nchi nne za Kiarabu, waziri wa mambo ya nje wa nchi hiyo amesema katika kumbukumbu ya mwaka mmoja tangu Doha ianze kuwekewa vikwazo, kwamba nchi nne za Saudia, Imarati, Misri na Bahrain ziache ndoto za alinacha na njozi zisizoagulika.
-
Waziri wa Ulinzi wa Qatar: Hatutashiriki katika vita vyovyote dhidi ya Iran
Jun 04, 2018 01:29Khalid bin Mohammad Al Attiyah, Naibu Waziri Mkuu wa Qatar ambaye pia ni Waziri wa Ulinzi wa nchi hiyo amesema kuwa nchi yake haitoshiriki katika vita vyovyote dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kuongeza kwamba, haamini kuwa Marekani pia itatekeleza vita vya namna hiyo dhidi ya Tehran.
-
Saudia yatishia kuishambulia kijeshi Qatar iwapo itanunua S-400 kutoka Russia
Jun 02, 2018 03:27Mfalme Salman Bin Abdul Aziz Aal-Saud wa Saudi Arabia ametishia kuwa Riyadh itachukua hatua za kijeshi dhidi ya Qatar iwapo serikali ya Doha itaendelea na mpango wake wa kununua mfumo wa makombora wa S-400 kutoka Russia.