Oct 08, 2020 14:13
Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limesema, Waislamu wapatao 130,000 wa jamii ya Rohingya waliosalia kwenye kambi za wakimbizi zilizoko kwenye jimbo la Rakhine nchini Myanmar wanaishi katika mazingira ya unyonge na udhalili. Human Rights Watch imeihimiza serikali ya nchi hiyo ikomeshe haraka uwekaji kizuizini huo wa kiholela na usio na mwisho wa watu hao.