-
Warohingya 60,000 wawasili Bangladesh kufuatia kupamba moto mzozo nchini Myanmar
Dec 23, 2024 14:12Huku kukiwa na mzozo kati ya serikali ya kijeshi na jeshi la waasi la Arakan nchini Myanmar, Waislamu wa kabila la Rohingya wapatao 60,000 wamewasili Bangladesh katika muda wa miezi miwili iliyopita.
-
Jumuiya ya kimataifa yahimizwa kuzidisha juhudi maradufu ili kuwasaidia wakimbizi wa Rohingya
Mar 14, 2024 06:58Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) na washirika wengine wa masuala ya kibinadamu jana waliitaka jamii ya kimataifa kuzidisha juhudi maradufu ili kuwalinda na kuwasaidia wakimbizi wa Rohingya na wenyeji wao.
-
Umoja wa Mataifa waomba misaada kwa ajili wakimbizi wa Rohingya
Dec 28, 2022 08:01Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi limeziomba msaada kwa nchi mbalimbali kwa ajili ya wakimbizi wa Rohingya baada ya Waislamu wasiopungua 20 wa jamii hiyo kuaga dunia baharini na mamia ya wengine kunusurika kifo katika ufuo wa Indonesia baada ya wiki kadhaa za kutangatanga katika Bahari ya Hindi.
-
Hatimaye Waislamu Warohingya wawasili pwani ya Indonesia baada ya kutaabika baharini kwa mwezi mzima
Dec 26, 2022 02:17Makumi ya Waislamu wakimbizi wa jamii ya Rohingya kutoka Myanmar waliodhoofu kwa njaa na kiu wamepatikana ufukweni mwa pwani ya jimbo la Aceh kaskazini ya Indonesia baada ya wiki kadhaa za kutaabika na kutangatanga baharini.
-
UN yataka dunia iwasaidie wakimbizi Waislamu wa Rohingya
Aug 26, 2022 07:25Mjumbe Maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametoa mwito kwa jamii ya kimataifa kuwasaidia kwa hali na mali wakimbizi Waislamu wa Rohingya walioko nchini Bangladesh.
-
Wanasheria wa Gambia: Kesi kuhusu mauaji ya kimbari ya Warohingya ni halali
Feb 24, 2022 15:05Wanasheria wa Gambaia wameitaka mahaka ya ngazi ya juu ya Umoja wa Mataifa kutupilia mbali ombi la kisheria la Myanmar la kuhitimishwa kesi inayoituhumu nchi hiyo ya kusini mashariki mwa Asia kuwa imefanya mauaji ya kimbari dhidi ya Waislamu wa kabila la Rohingya baada ya nchi hiyo ya Kibuda kufanya kila iwezalo kuifutilia mbali kesi hiyo.
-
Wapinzani wa utawala wa kijeshi Myanmar watangaza mshikamano na Waislamu wa Rohingya
Jun 14, 2021 08:17Wapinzani wa utawala wa kijeshi nchini Myanmar wameanzisha kampuni ya kuonyesha mshikamano wao na Waislamu wa jamii ya Rogingya wanaodhulumiwa na kukandamizwa nchini humo.
-
Bangladesh yachunguza mkasa wa moto ulioua Waislamu 15 wa Rohingya
Mar 24, 2021 02:48Serikali ya Dhaka imeanzisha uchunguzi kubaini kiini cha moto mkubwa uliotokea katika kambi ya wakimbizi Waislamu wa jamii ya Rohingya katika wilaya ya Cox's Bazar nchini Bangladesh na kuua na kujeruhi mamia ya watu.
-
The Observer yahoji: Walikuwa wapi waandamanaji wa sasa huko Myanmar wakati wa mauaji ya kimbari dhidi ya Waislamu wa Rohingya?
Feb 23, 2021 02:48Gazeti la The Observer linalochapishwa nchini Uingereza limeandika makala kuhusu maandamano makubwa yanayoendelea nchini Myanmar kupinga mapinduzi ya kijeshi yaliyoiondoa madarakani serikali iliyochaguliwa kwa njia za kidemokrasia na kuhoji kuwa, walikuwa wapi waandamanaji hao katika kipindi chote cha miaka minne ya mauaji ya kimbari yanayofanywa na jeshi la nchi hiyo likishirikiana na Mabudha wenye misimamo mikali dhdi ya Waislamu wa jamii ya Rohingya?
-
HRW: Waislamu Warohingya wanaishi kwenye 'jela ya wazi' na katika "unyonge na udhalili"
Oct 08, 2020 14:13Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limesema, Waislamu wapatao 130,000 wa jamii ya Rohingya waliosalia kwenye kambi za wakimbizi zilizoko kwenye jimbo la Rakhine nchini Myanmar wanaishi katika mazingira ya unyonge na udhalili. Human Rights Watch imeihimiza serikali ya nchi hiyo ikomeshe haraka uwekaji kizuizini huo wa kiholela na usio na mwisho wa watu hao.