Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limesema mashambulizi ya anga yaliyofanywa hivi karibuni na jeshi la Myanmar katika mkoa wa Rakhine na kuua idadi kubwa ya raia wakiwemo watoto wadogo ni jinai za kivita.
Shirika la kutetea haki za binadmau la Human Rights Watch (HRW) limetoa mwito wa kufanyika uchunguzi baada ya picha za satalaiti kuonyesha nyumba za Waislamu katika mkoa wa Rakhine nchini Mynamar zikiteketea kwa moto.
Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya haki za binadamu nchini Myanmar amelituhumu jeshi la nchi hiyo kuwa lingali linawatendea jinai za kivita na zilizo dhidi ya binadamu Waislamu wa jamii ya Rohingya katika majimbo mawili ya nchi.
Makumi ya Waislamu wa jamii ya Rohingya wamepoteza maisha kutokana na njaa baada ya boti yao kukwama baharini kwa majuma kadhaa.
Kwa akali Waislamu 16 wa jamii ya Rohingya wamefariki dunia baada ya boti yao kuzama katika Pwani ya Bengal, kaskazini mwa Bangladesh.
Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) imepongeza agizo la Mahakama ya Kimataifa ya Uadilifu (ICJ) lilioitaka serikali ya Myanmar kuchukua hatua za dharura za kuzuia mauaji ya kimbari ya Waislamu wa Rohingya na kubainisha kwamba, serikali ya Myanmar inapaswa kuheshimu agizo hilo.
Kituo cha habari cha Middle East Eye kimeripoti kuwa, Saudi Arabia inazidisha mashaka na masaibu ya Waislamu wa jamii ya Rohingya huko Myanmar kwa kuwasaka, kuwakamata na kuwafukuza Warohingya wanaofanya kazi nchini humo.
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limepasisha azimio ambalo linailaani vikali Myanmar kwa ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu dhidi ya Waislamu wa jamii ya Rohingya na jamii za wengine waliowachache katika nchi hiyo ya Mabuddha.
Wananchi wa Uholanzi wamefanya maandamano katika mji wa Hague wakipinga mauaji ya kimbari yanayofanywa na Mabudha wenye misimamo mikali wakishirikiana na jeshi la Myanmar dhidi ya Waislamu wa jamii ya Rohingya.
Mahakama ya Kimataifa ya Uadilifu (ICJ) imeanza kusikiliza kesi kuhusu mauaji ya kimbari ya Waislamu wa Myanmar kufuatia shtaka ambalo limewasilishwa na Gambia.