Oct 05, 2019 12:23
Mchunguzi huru wa Umoja wa Mataifa kuhusu Myanmar amesema mamia ya maelfu ya Waislamu wa jamii ya Rohingya waliorejea mkoani Rakhine wakitokea Bangladesh wanakandamizwa na kuandamwa na kila aina ya dhuluma na kwa msingi huo, Myanmar sio salama kwa Warohingya zaidi kurejea.