Sep 26, 2018 04:07
Baada ya kunyamaza kimya kwa muda mrefu mbele ya jinai na mauaji ya kimbari yanayofanywa dhidi ya Waislamu wa jamii ya Rohingya nchini Myanmar, hatimaye Marekani imetoa ripoti ikisisitiza kuuwa jeshi la nchi hiyo ya Kusini Mashariki mwa Asia limefanya jinai na uhalifu wa kupanga na ulioratibiwa dhidi ya jamii hiyo.