-
Rouhani na Erdogan walaani msimamo wa US, Israel dhidi ya Iran
Jan 03, 2018 23:05Marais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Uturuki wamekosoa vikali uchochezi na uungaji mkono wa Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel kwa waandamanaji wanaofanya fujo na ghasia nchini.
-
Rais Rouhani: Maadui wamekasirishwa na maendeleo ya Iran
Jan 01, 2018 12:43Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa mafanikio ya taifa la Iran katika nyanja mbalimbali za kiuchumi, kisiasa na kikanda yamewatia hasira na kuwaghadhibisha maadui.
-
Rais Rouhani: Marekani haina haki ya kujifanya ina uchungu na taifa la Iran
Jan 01, 2018 01:04Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, rais wa Marekani ambaye miezi kadhaa iliyopita aliwatuhumu watu wa taifa la Iran kuwa ni magaidi, hana haki ya kujifanya ni mwenye uchungu na nchi hii.
-
Rais wa Iran atuma salamu za pongezi kwa mnasaba wa kuadhimisha kuzaliwa Nabii Isa AS
Dec 24, 2017 23:53Rais Hassan Rouhani amemtumia salamu viongozi wa mataifa ya dunia na kuwapa mkono wa pongezi kwa mnasaba wa kuadhimisha kuzaliwa mtume wa rehma na saada Nabii Isa Masih AS na vilevile kwa kukaribia kuanza mwaka mpya wa 2018 miladia.
-
Rais Rouhani: Marekani haiwezi kubatilisha mapatano ya nyuklia ya JCPOA
Dec 19, 2017 10:39Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema tokea yaanze kutekelezwa mapatano ya nyuklia ya Iran yanayojulikana kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezwaji, JCPOA, Marekani imetaka mara kadhaa mapatano hayo yabatilishwa lakini haiwezi kufanikiwa katika hilo.
-
Rais Rouhani: Waislamu wakabiliane na uamuzi wa Trump kuhusu Quds
Dec 13, 2017 13:00Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametoa mapendekezo 8 kwa ulimwengu wa Kiislamu kwa ajili ya kukabiliana na uamuzi usio sahihi na kinyume cha sheria uliochukuliwa na Rais Donald Trump wa Marekani kuhusu Quds tukufu na kusema kuwa: Marekani inafuatilia maslahi ya Wazayuni na haiheshimu matakwa halali ya Wapalestina.
-
Rouhani: Uamuzi wa Trump dhidi ya Quds ni sehemu ya njama za Wazayuni, Wamarekani dhidi ya Ulimwengu wa Kiislamu
Dec 12, 2017 13:13Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameutaja kuwa wa kijuba na ulio kinyume cha sheria uamuzi wa Rais wa Marekani kuhamisha ubalozi wa nchi hiyo kutoka Tel Aviv hadi Quds Tukufu na kuongeza kuwa: "Mpango huu ni sehemu ya njama za Wazayuni na Wamarekani dhidi ya Ulimwengu wa Kiislamu."
-
Rouhani: Mataifa ya Kiislamu yatazima njama ya Marekani na Israel
Dec 11, 2017 23:30Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema umoja, muqawama na mapambano ya Wapalestina na nchi nyingine za Kiislamu bila shaka yatapelekea kusambaratika kwa njama ya Marekani na utawala wa Kizayuni ya kuitambua Quds tukufu kuwa 'mji mkuu' wa utawala haramu wa Israel.
-
Rais wa Iran: Uamuzi usio sahihi wa Trump ni sawa na kumwagia petroli kwenye moto
Dec 10, 2017 13:05Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, uamuzi wa hivi karibuni wa Rais Donald Trump wa Marekani wa kuitangaza Beitul-Muqaddas kuwa mji mkuu wa Israel na kutoa amri ya kuhamishiwa ubalozi wa Washington katika mji huo ulikuwa sawa na kumwagia mafuta ya petroli katika moto katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
Si muhali Iran kuwa na uhusiano mzuri na Saudia ikiacha mauaji Yemen, kukata uhusiano na Israel
Dec 10, 2017 04:29Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema taifa hili litaacha kuwa na msuguano na Saudi Arabia iwapo Riyadh itaacha kuwashambuliwa kwa mabomu wananchi wasio na hatia wa Yemen sambamba na kukata uhusiano na utawala wa Kizayuni wa Israel.