-
Russia yaponda madai ya Marekani dhidi ya Syria
Feb 03, 2018 23:13Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia imekadhibisha madai ya Marekani kwamba Syria imetengeneza na kutumia kizazi kipya cha silaha za kemikali na kusema madai hayo hayana msingi wowote.
-
Radiamali ya Russia kwa tuhuma za Waziri wa Ulinzi wa Uingereza
Jan 27, 2018 00:46Wizara ya Ulinzi ya Russia imetangaza kuwa, tuhuma zilizotolewa na Waziri wa Ulinzi wa Uingereza dhidi ya Russia ni za uongo.
-
Russia na Syria zakanusha madai ya Marekani kuhusu silaha za kemikali
Jan 24, 2018 23:27Russia na Syria zimekadhibisha madai yaliyotolewa na Marekani na Ufaransa kwamba serikali ya Damascus imetumia silaha za kemikali katika mashambulizi yake, zikisisitiza kuwa tuhuma hizo zinapania kutia vizingiti katika juhudi za kupatiwa ufumbuzi kwa njia ya amani mgogoro unaoshuhudiwa katika nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Russia: Habari kwamba tunataka kufungua kambi za kijeshi Libya na Misri ni uongo
Jan 13, 2018 10:32Mkuu wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Baraza la Shirikisho la Russia amesema kuwa, serikali ya Moscow, haina nia yoyote ya kuanzisha kambi za kijeshi katika nchi za Misri na Libya.
-
Njama za kuvuruga muungano wa vita dhidi ya ugaidi wa Iran, Russia na Uturuki
Jan 13, 2018 04:09Nchi za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Russia na Uturuki zina muungano ambao si tu kuwa umeweza kufanikiwa katika medani ya vita dhidi ya ugaidi, bali pia katika mazungumzo ya kidiplomasia, muungano huo umeweza kuibua mabadiliko katika masuala yanayohusiana na tatizo la ugaidi.
-
Assad: Njama za adui za kuigawa Syria zimegonga mwamba
Jan 13, 2018 00:15Rais wa Syria ameeleza kuwa ushindi wa jeshi la nchi hiyo umepelekea kuandaliwa njia ya kurejesha amani nchini humo.
-
Rais Putin: Kiongozi wa Korea Kaskazini ni mtu mwenye uwezo mkubwa wa akili
Jan 12, 2018 01:07Rais Vladmir Putin wa Russia amesema kuwa, Kim Jong-un Kiongozi wa Korea Kaskazini, ni mtu mwenye uwezo mkubwa wa akili na aliyepikika.
-
Russia yalitaka Baraza la Usalama liingilie kati kuhusu hatua ya Marekani huko Raqqah Syria
Jan 10, 2018 04:28Mwakilishi wa Russia katika Umoja wa Mataifa ameliomba Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lichukue hatua kuhusu hali ya kibinadamu inayoshuhudiwa sasa huko Raqqah Syria na kuchukua uamuzi kuhusu hatua zinazotekelezwa na Marekani katika mji huo baada ya kukombolewa kutoka mikononi mwa magaidi wa kundi la Daesh.
-
Iran, Russia zalitaka Baraza la Usalama lisifuate mashinikizo ya Marekani
Jan 06, 2018 03:54Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Russia zimekosoa udhaifu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wa kukubali mashinikizo ya Marekani ya kuitisha kikao cha dharura kuhusu maandamano ya hivi karibu nchini Iran.
-
Kuanza tena safari za ndege kati ya Russia na Misri
Jan 04, 2018 10:19Rais wa Russia amesaini dikrii akiamuru kuanza tena safari za kawaida za ndege kati ya nchi hiyo na Misri ambazo zilisimamishwa kufuatia mlipuko uliotokea katika ndege ya Russia katika anga ya mkoa wa Sinai kaskazini mwa Misri.