Oct 13, 2018 07:41
Sera za kujichukulia maamuzi ya upande mmoja za Rais Donald Trump wa Marekani zimeifanya nchi hiyo iendelee kutengwa duniani. Katika kutekeleza kaulimbiu yake ya "Marekani Kwanza", Trump, mbali na kuyapa kipaumbele cha kwanza maslahi na malengo ya Marekani, tab'an bila kujali nafasi za nchi zingine, anaitakidi kuwa siasa na sera za ubinafsi na uchukuaji maamuzi ya upande mmoja zitaongeza nguvu za Marekani na kuiwezesha kuwashinda washindani wake.