-
Wanaokaidi karantini ya corona Kigali Rwanda, kukiona + Sauti
Jan 21, 2021 18:08Siku tatu baada ya mji mkuu wa Rwanda Kigali kuwekwa kwenye zuio la wakazi wake kukaa nyumbani, baadhi ya wananchi wameonekana kukaidi miito hiyo na polisi wameonya kuwachukulia hatua kali ikiwa wataendelea kufanya hivyo. Serikali ya Rwanda iliamua kuweka zuio la wiki mbili kwa wakazi wa mji mkuu Kigali kutokana na ongezeko la maambukizi ya kirusi cha corona. Kutoka Kigali mwandishi wetu Sylivanus Karemera anaripoti zaidi.
-
Rwanda na Malawi zafunga shule tena baada ya maambukizo ya corona kuongezeka
Jan 18, 2021 11:52Serikali za Rwanda na Malawi kuanzia leo Jumatatu zimefunga shule zikiwemo za chekechea kutokana na ongezeko la kesi za maambukizi ya ugonjwa wa Covid-19 katika nchi hizo.
-
Rwanda yazinduwa maabara ya kupima COVID-19 katika uwanja wa ndege wa Kigali
Dec 26, 2020 07:27Wizara ya Afya ya Rwanda imezindua maabara ya kupima COVID-19 katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kigali ili kurahisisha utoaji wa huduma kwa wageni wanaoingia Rwanda.
-
Vipimo vya COVID-19 kupatikana kwa wingi na rahisi nchini Rwanda + Sauti
Dec 18, 2020 13:25Serikali ya Rwanda imeziruhusu zahanati zote binafsi nchini humo kupima maambukizo ya kirusi cha corona tena kwa kutumia vifaa vya kisasa zaidi vinavyotoa majibu chini ya dakika 15. Rwanda inasema inafanya hivyo kukabiliana na kasi ya ongezeko zaidi la wagonjwa wa COVID-19 nchini humo. Kutoka Kigali mwandishi wetu Sylivanus Karemera anaripoti zaidi.
-
Vita vya kupambana na rushwa vinaendelea nchini Rwanda + Sauti
Dec 10, 2020 16:45Serikali ya Rwanda imesema kuwa, utashi wa serikali na mikakati inayoendelea kuwekwa, ndivyo vitakavyokuwa suluhisho la kutokomeza ulaji rushwa nchini humo. Licha ya Rwanda kutajwa na mashirika ya kimataifa kuwa miongoni mwa nchi zinazofanya vizuri kwenye mapambano ya ulaji rushwa lakini bado nchi hiyo inasema juhudi kali za kuikabili rushwa zitaendelea. Kutoka Kigali mwandishi wetu Sylivanus Karemera anaripoti zaidi…
-
Wamarekani wenye asili ya Afrika wapatao 100 waiomba serikali ya Rwanda idhini ya kuishi nchini humo + SAUTI
Dec 08, 2020 16:32Wamarekani wenye asili wapatao 100 wameiomba serikali ya Rwanda idhini ya kuishi nchini humo
-
Kabuga afikishwa katika Mahakama ya Umoja wa Mataifa, asema hana hatia
Nov 12, 2020 04:21Mshukiwa wa mauaji ya kimbari nchini Rwanda, Felicien Kabuga jana Jumatano alifikishwa katika Mahakama ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania ambapo alisisitiza kuwa hana hatia katika mashitaka ya jinai yanayomkabili.
-
Jeshi la Rwanda lakamata wanamgambo 19 wa Burundi mpakani
Oct 04, 2020 07:35Jeshi la Ulinzi la Rwanda (RDF) limewatia mbaroni wanamgambo 19 wa Burundi waliokuwa wamejizatiti kwa silaha katika mpaka wa nchi mbili hizo jirani.
-
Rusesabagina asema alihadaiwa na kupelekwa Rwanda badala ya Burundi
Sep 18, 2020 10:41Paul Rusesabagina anayejulukana kama Shujaa wa filamu ya 'Hotel Rwanda' inayosimulia kisa cha mauaji ya kimbari ya mwaka 1994 nchini Rwanda, anasema kuwa, aliamini alikuwa akisafiri kwenda Burundi kwa mwaliko wa mchungaji wa kanisa, lakini badala yake akahadaiwa na kupelekwa Rwanda na kukamatwa kwa tuhuma za ugaidi.
-
Shujaa wa filamu ya 'Hotel Rwanda' afikishwa mahakamani kwa makosa ya ugaidi, mauaji
Sep 14, 2020 11:27Shujaa wa filamu ya 'Hotel Rwanda' inayosimulia kisa cha mauaji ya kimbari ya mwaka 1994 nchini Rwanda, Paul Rusesabagina, leo Jumatatu amefikishwa mahakamani mjini kigali akikabiliwa na mashtaka ya ugaidi, kufadhili ugaidi mauaji na kuteka nyara.