-
Ripoti: Mamia ya Wanawafalme Saudia wanaugua corona
Apr 18, 2020 07:09Kuna idadi kubwa ya wanawafalme katika Ufalme wa Saudi Arabia ambao wanaugua ugonjwa wa corona au COVID-19, na idadi yao kamili ni kubwa kuliko ile inayotangazwa na vyombo husika.
-
Maseneta wa Marekani watishia 'kuichukulia hatua' Saudia
Apr 11, 2020 09:19Maseneta wa Marekani wametishia kuangalia upya uhusiano wao na Saudi Arabia kutokana na hatua ya Riyadh ya kuendelea kuvutana na Russia juu ya bei ya mafuta ghafi ambayo imeiathiri pia Marekani.
-
Saudia inawatuma Yemen watu walioathirika na virusi vya Corona
Apr 10, 2020 23:55Katibu Mkuu wa Baraza Kuu la Uratibu wa Masuala ya Haki za Binaadamu nchini Yemen amesisitiza kuwa, Saudi Arabia imekuwa ikituma waathirika wa virusi vya Corona Yemen na kwamba vyombo vya usalama vya nchi hiyo vinafanya juhudi kubwa kuweza kuwatambua watu hao.
-
Muungano vamizi wa kijeshi unaoongozwa na Saudia waendelea kukiuka usitishaji vita nchini Yemen
Apr 10, 2020 07:29Huku Martin Griffiths, Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Yemen na Nayef Falah al Hajraf, Katibu Mkuu wa Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi wakipongeza uamuzi wa kusitisha vita na mapigano nchini Yemen, muungano vamizi unaoongozwa na Saudia katika vita huko Yemen umeendelea kukiuka usitishaji vita huo.
-
Human Rights Watch yakosoa kamatakamata ya wanaharakati nchini Saudia
Mar 18, 2020 03:57Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limetoa taarifa likikosoa hatua ya serikali ya Saudi Arabia ya kuwatia nguvuni maafisa wa serikali, wanaharakati na wakosoaji wa utawala wa nchi hiyo.
-
Hamas yalaani kuendelea kushikiliwa Wapalestina nchini Saudi Arabia
Mar 09, 2020 04:26Msemaji wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amelaani kutiwa mbaroni viongozi wa Wapalestina na kupandishwa kizimbani huko Saudi Arabia.
-
Shirika la ESOHR laionya Saudia isitekeleze hukumu ya kifo dhidi ya vijana watano
Mar 03, 2020 08:31Shirika moja la haki za binaadamu la barani Ulaya limetoa taarifa na kufichua kwamba Saudia inakusudia kutekeleza adhabu ya kifo dhidi ya vijana watano ambao iliwakamata wakiwa bado na umri mdogo.
-
Senegal na Saudia zaripoti kesi za kwanza za Corona, waliofariki Marekani wafika 6
Mar 03, 2020 04:00Saudi Arabia, Jordan na Tunisia ni nchi za hivi punde katika ulimwengu wa Kiarabu kuripoti kesi za kwanza za virusi vya Corona ambavyo vimeshaua watu zaidi ya elfu tatu kote duniani, hususan nchini China.
-
Kuhani mmoja Myahudi-Mzayuni akutana na mfalme wa Saudi Arabia
Feb 22, 2020 03:56Wizara ya Mambo ya Nje ya utawala wa Kizayuni wa Israel imetangaza kuwa, kuhani mmoja Mzayuni ameonana na mfalme wa Saudi Arabia mjini Riyadh.
-
Ujerumani yaitaka Saudi Arabia ichunge haki za binadamu
Feb 22, 2020 03:50Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani amewataka viongozi wa Saudi Arabia wafanyie marekebisho sheria zao na wachunge haki za binadamu.