-
Iran yasisitiza haingilii mambo ya ndani ya nchi nyingine
Nov 13, 2017 12:04Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema: "Sera ya kimsingi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni kutoingilia kamwe masuala ya ndani ya nchi nyingine."
-
Rais wa Lebanon: Matamshi ya Saad Hariri hayana itibari
Nov 13, 2017 04:48Rais Michel Aoun wa Lebanon amesema: Saad Hariri, tangu siku ya Jumamosi hadi sasa yuko nchini Saudi Arabia katika mazingira tata na yasiyoeleweka; na misimamo yake ni misimamo ya kutia shaka na kutatanisha.
-
Hariri ajidhalilisha Saudia, apanga foleni kumpa mkono Mfalme Salman
Nov 12, 2017 10:18Kanda ya video iliyorushwa hewani na televisheni ya utawala wa Aal-Saud imemuonyesha Waziri Mkuu wa Lebanon aliyetangaza kujiuzulu hivi karibuni akijidhalilisha kwa kupanga foleni na maafisa wa serikali ya Riyadh kwa ajili ya kumpa mkono Mfalme Salman Bin AbdulAzizi wa Saudi Arabia.
-
Tunisia yaikosoa Saudia kwa hatua zake za kuzusha migogoro katika nchi nyingine
Nov 12, 2017 04:19Waziri Mkuu wa Tunisia ametoa radiamali yake kutokana na hatua ya kuibua migogoro ya Saudia katika nchi nyingine hususan Lebanon na kuonyesha matarajio kwamba mzozo huo hautapelekea kutokea vita kati ya nchi mbili.
-
Rais wa Uturuki akosoa kauli ya Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa Saudi kuhusu Uislamu
Nov 12, 2017 04:08Katika msururu wa kurushiana maneneo viongozi wa Saudi Arabia na Uturuki, Rais Reccep Tayyip Erdogan wa Uturuki amekosoa vikali matamshi ya Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa Saudia Mohammad Bin Salman kuhusu kile alichodai kuwa ni "Uislamu wa misimamo ya wastani."
-
Maafisa wa ngazi za juu wa Saudi Arabia na Israel wakutana Marekani
Nov 12, 2017 01:16Tzipi Livni Waziri wa zamani wa mambo ya nje wa utawala wa Kizayuni wa Israel amekutana na Turki al Faisal, mkuu wa zamani wa shirika la kijasusi la Saudi Arabia.
-
Iran: Saudia ni dhihirisho la ugaidi na kuingilia masuala ya ndani ya nchi nyingine
Nov 12, 2017 01:03Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa, Saudia ndio dhihirisho la misimamo ya kufurutu ada na ugaidi na kuingilia masuala ya ndani ya nchi nyingine, lakini inazituhumu nchi nyiengine kuwa zinaunga mkono ugaidi.
-
Yemen: Madai ya Marekani kuwa Iran imehusika katika shambulizi la Riyadh ni kichekesho
Nov 11, 2017 12:18Wizara ya Mambo ya Nje ya Yemen imekadhibisha madai ya Marekani kwamba Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ilihusika katika shambulizi la kombora la Burkan 2 kutoka Yemen kwenda Riyadh na imeyataja madai hayo kuwa ni kichekesho.
-
Hitilafu za kimitazamo kati ya Trump na Tillerson kuhusu matukio ya Saudia
Nov 11, 2017 08:22Matukio yanayojiri nchini Saudi Arabia kwa mara nyingine tena yameweka wazi hitilafu zilizopo kati ya Rais wa Marekani na Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya nchi hiyo.
-
UNICEF: Mzingiro wa Saudia utaua maelfu ya watoto Wayemen wenye njaa
Nov 10, 2017 11:38Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuwahudumia Watoto UNICEF limeonya kuhusu madhara makubwa ya mzingiro wa Saudi Arabia dhidi ya Yemen na kusema idadi kubwa ya watoto Wayemen wanaweza kupoteza maisha kwani tayari wanakabiliwa na lishe duni.