-
Qatar yaafiki upatanishi wa Kuwait katika mgogoro na Saudia
Jun 06, 2017 09:10Qatar imesema iko tayari kuipa Kuwait fursa kuwa mpatanishi katika mgogoro ulioibuka baada ya Saudi Arabia kuzichochea nchi kadhaa za Kiarabu kukata uhusiano na nchi hiyo.
-
Qatar: Madai dhidi yetu si ya kweli na hayana msingi
Jun 05, 2017 03:15Baada ya Saudi Arabia, Misri, Imarati na Bahrain kukata uhusiano na Qatar mapema leo Jumatatu, wizara ya mambo ya nje wa Qatar imesema, imesikitishwa na hatua hiyo.
-
Kiongozi wa upinzani Uingereza aituhumu Saudia kwa kuunga mkono ugaidi
Jun 05, 2017 02:20Kiongozi wa upinzani nchini Uingereza, Jeremy Corbyn amesema, wakati sasa umewadia kwa nchi yake kufanya 'mazungumzo magumu' na Saudia Arabia na madola mengine ya Kiarabu ambayo yanaunga mkono magaidi.
-
Wapiganaji wa Ansarullah wamuangamiza afisa wa jeshi la Saudia
Jun 03, 2017 10:39Wapiganaji wa Harakati ya Ansarullah nchini Yemen wamepambana vikali na wanajeshi vamizi wa Saudi Arabia katika maeneo ya mipakani na kumuangamiza afisa wa jeshi la Saudia mwenye cheo cha kapteni.
-
Saudia yatabiri kutokea mapinduzi ya kijeshi nchini Qatar
Jun 02, 2017 21:59Katika hali inayoonekana ni ya kuzidi kuvurugika uhusiano wa Saudi Arabia na Qatar, gazeti moja la Saudia linalochapishwa mjini Riyadh limetabiri kuwa, kuna uwezekano wa kutokea mapinduzi ya sita ya kijeshi nchini Qatar hasa kwa kuzingatia katika nchi hiyo ndogo ya Kiarabu kumetokea mapinduzi matano ya kijeshi katika kipindi cha baina ya mwaka 1971 na 2013.
-
Utawala wa Aal-Saud watumia ndege zisizo na rubani kushambulia raia eneo la Qatif
Jun 01, 2017 23:50Vyombo vya habari nchini Saudi Arabia vimetangaza kuwa, utawala wa Aal-Saud umetumia ndege zisizo na rubani katika mashambulizi dhidi ya raia katika eneo la Qatif, mashariki mwa nchi hiyo.
-
Wasomi 1500 wa Misri wapinga kupewa Saudia visiwa vya nchi yao
Jun 01, 2017 09:51Shakhsia na wasomi 1500 wa Misri wametangaza rasmi upinzani wao kwa uamuzi wa serikali ya nchi hiyo wa kutaka kuipa Saudi Arabia visiwa viwili vya Misri vya Tiran na Sanafir.
-
Abdul-Malik al-Houthi: Fikra za Uwahabi za Saudia ndizo zinazoeneza ugaidi duniani
Jun 01, 2017 02:58Katibu Mkuu wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen amekosoa vikali misimamo ya Saudi Arabia na mkatakati wake wa kueneza fikra za Uwahabi na kubainisha kwamba, matukio ya kigaidi yanayoshuhudiwa katika maeneo mbalimbali duniani chimbuko lake ni fikra za Kiuwahabi za Saudia.
-
Mamluki 46 wa Saudia wauawa na kujeruhiwa Yemen
May 31, 2017 10:06Duru za kuaminika za Yemen zimetangaza habari ya kuuawa na kujeruhiwa karibu mamluki 46 wa Saudi Arabia katika mapigano na jeshi la Yemen.
-
Israel yafaidika na mkataba wa silaha wa Saudia, Marekani
May 29, 2017 03:16Gazeti moja la Kizayuni, limefichua kuwa, katika mkataba wa mabilioni ya dola wa ununuzi silaha baina ya Marekani na Saudia, mashirika ya Israel yatapata faida kubwa sana.