-
Umoja wa Afrika na Somalia kutathmini hatima ya AMISOM
Jan 01, 2022 04:26Somalia na Umoja wa Afrika (AU) zimekubaliana kutathmini operesheni za vikosi vya nchi wanachama wa umoja huo AMISOM, ambavyo muda wake uliongezwa mpaka mwezi Machi mwaka 2022.
-
AU yataka pande hasimu za kisiasa Somalia zifanye mazungumzo
Dec 31, 2021 23:31Umoja wa Afrika umetoa mwito kwa Rais Mohamed Abdullahi Farmaajo wa Somalia na Waziri Mkuu wa nchi hiyo aliyesimamishwa kazi hivi karibuni, Mohamed Hussein Roble kufanya mazungumzo haraka iwezekanavyo, baada ya wawili hao kutofautiana vikali wakati huu wa kuendelea uchaguzi wa bunge.
-
Financial Times latahadharisha: Ash-Shabaab wanaweza kurudi tena madarakani Somalia
Dec 30, 2021 08:10Gazeti la Financial Times limetahadharisha kuwa, kundi la kigaidi la Ash-Shabaab linaweza likarudi upya kwenye medani na kuidhibiti tena Somalia.
-
Rais wa Somalia amfuta kazi Waziri Mkuu wake, mzozo wapamba moto.
Dec 27, 2021 03:33Rais wa Somalia amemfuta kazi Waziri Mkuu wake wakati huu wa kuendelea uchaguzi wa bunge na hivyo kuzusha mzozo mpya wa kisiasa katika nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
5 wauawa katika shambulio la bomu la al-Shabaab kusini mwa Somalia
Dec 05, 2021 23:47Watu wasiopungua watano wameuawa katika mripuko wa bomu uliotokea katika mgahawa mmoja wenye shughuli nyingi kusini mwa Somalia.
-
Al-Shabaab yashambulia askari wa Ethiopia, uwanja wa ndege Somalia
Dec 01, 2021 00:13Kundi la kigaidi la al-Shabaab limeshambulia uwanja wa ndege na kambi ya kijeshi ya askari wa Ethiopia katika mji wa Baidoa, ulioko kusini magharibi mwa mji mkuu wa Somalia, Mogadishu.
-
Watu watano waaga dunia katika mlipuko wa bomu karibu na shule huko Mogadishu
Nov 25, 2021 04:45Watu watano wameuawa na wengine zaidi ya 12 wamejeruhiwa hii leo katika mlipuko wa bomu lililokuwa limetegwa ndani ya gari karibu na shule moja katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu.
-
Mwanahabari mtajika wa redio ya Somalia auawa katika shambulio la kigaidi
Nov 21, 2021 04:49Kundi la kigaidi la al Shabaab lenye mfungamano na mtandao wa al Qaida limehusika katika mlipuko wa bomu uliosababisha kifo cha mwandishi habari mtajika wa redio ya serikali ya Somalia huko Mogadishu.
-
Askari 2 wa Uganda wahukumiwa kifo kwa mauaji ya raia Somalia
Nov 14, 2021 04:46Askari wawili wa Jeshi la Ulinzi la Uganda (UPDF) wanaohudumu kwenye Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia (AMISOM) wamehukumiwa kifo, kutokana na mauaji ya raia katika nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
Jeshi la Somalia laangamiza magaidi 9 wa al-Shabaab kusini mwa nchi
Nov 11, 2021 00:44Jeshi la Taifa la Somalia (SNA) limetangaza kuwa limeua magaidi tisa wa kundi la al-Shabaab katika wilaya ya Awdhigle kusini mwa nchi hiyo.