-
Afisa wa serikali afukuzwa kazi kwa kutaka Somalia iwe na uhusiano na Israel
Apr 01, 2019 20:25Serikali ya Somalia imempiga kalamu nyekundu Mkurugenzi katika Wizara ya Mambo ya Nje ya nchi hiyo, kwa kutoa mwito wa kuwepo uhusiano wa kidiplomasia kati ya nchi hiyo ya Pembe ya Afrika na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Kiongozi mwandamizi wa kundi la kigaidi la Al Shabab ajisalimisha Somalia
Mar 31, 2019 22:25Kiongozi wa ngazi za juu wa kundi la kigaidi la Al Shabab amejisalimishwa kwa askari wa serikali ya Somalia katika mji wa Marka katika eneo la kusni mwa nchi hiyo la Lower Shabelle.
-
Watu 15 wauawa katika shambulizi la kigaidi Mogadishu, Somalia
Mar 28, 2019 10:38Kwa akali watu 15 wameuawa katika mripuko wa bomu lililokuwa limetegwa garini, nje ya hoteli na mikahawa katika eneo lenye shughuli nyingi katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu.
-
Kikosi cha Umoja wa Mataifa Somalia, UNSOM, chaongezewa muda wa kuhudumu
Mar 28, 2019 03:30Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limepitisha azimio la kuongeza muda wa kuwepo kwa Kikosi cha Kutoa Msaada cha Umoja wa Mataifa nchini Somalia UNSOM hadi tarehe 31, Machi mwaka 2020.
-
Waziri ni miongoni mwa watu 15 waliouawa katika shambulizi la kigaidi Somalia
Mar 23, 2019 22:42Kwa akali watu 15 wameuawa katika shambulizi la kigaidi la jana Jumamosi katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu.
-
Milipuko ya mabomu na milio ya risasi vyautikisa mji wa Mogadishu Somalia
Mar 23, 2019 09:45Duru za habari nchini Somalia zimeripoti kuwa miripuko miwili ya kutisha ya mabomu pamoja na milio ya risasi imeitikisa Mogadishu, mji mkuu wa Somalia.
-
Wanajeshi wa Somalia wagoma kwa kutolipwa mishahara ya miezi minne
Mar 21, 2019 11:24Azma ya Somalia ya kusimamia usalama wake pasi na kutegemea uungaji mkono wa Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Afrika (Amisom) imekumbwa na kizingiti, baada ya baadhi ya askari wa Somalia kufanya mgomo kulalamikia kutolipwa mishahara yao kwa miezi kadhaa sasa.
-
Amnesty International: Marekani inahusika katika kuwaua raia wa Somalia
Mar 21, 2019 00:17Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limesema kuwa, jeshi la Marekani linahusika katika mauaji ya raia wa Somalia kupitia mashambulizi yake ya ndege zisizo na rubani nchini humo.
-
Magaidi 19 wa al-Shabaab waangamizwa nchini Somalia
Mar 14, 2019 10:40Wanachama wasiopungua 16 wa kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab wameuawa katika makabiliano baina ya kundi hilo na vikosi vya usalama katika eneo la Bar Sanguni na Jamame mkoani Lower Juba, kusini mwa Somalia.
-
Mlipuko wa bomu waua watu wanane katika soko la mnada wa mifugo Somalia
Mar 14, 2019 04:37Kwa akali watu wanane wameuawa nchini Somalia na makumi ya wengine kujeruhiwa baada ya kutokea mlipuko wa bomu katika soko la kuuza na kununua mifugo kusini magharibi mwa nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.