AMISOM yakanusha madai ya Al Shabab kuuteka mji wa kistratijia
Kikosi cha Kijeshi cha Umoja wa Afrika nchini Somalia (AMISOM) kimekanusha habari kuwa kundi la kigaidi la al-Shabab limetwaa tena mji wa Sabiid kwenye wilaya ya kusini uliokombolewa hivi karibuni.
AMISOM imethibitisha kuwa mji wa Sabiid bado unadhibitiwa na Jeshi la Serikali ya Somalia linaloungwa mkono na AMISOM. Mjio huo muhimu kistratijia uko umbali wa kilomita 40 kusini mwa mji mkuu Mogadishu
AMISOM imesema vikosi vya ushirikiano vitaendelea kusimamia amani nchini Somalia, na kupuuza habari kuhusu kuchukuliwa kwa mji wa Sabiid kama propaganda za al-Shabab.
Umoja wa Mataifa unafadhili askari hao wa Amisom ambao sasa ni 21,000 na wamekuweko nchini Somalia tokea mwaka 2007. Wanajeshi wa Amisom walioko Somalia ni kutoka Uganda, Kenya, Burundi, Somalia, Ethiopia, Djibouti na Sierra Leone. Nao maafisa wa polisi wa AMISOM ni kutoka Nigeria, Sierra Leone na Uganda.