-
AU yasisitiza haja ya kumalizwa vita na kuanza mazungumzo nchini Sudan
Apr 28, 2023 22:21Umoja wa Afrika AU umesisitizia haja ya kumalizwa mzozo nchini Sudan na kuanza tena mazungumzo kati ya pande hizo mbili zinazozozana.
-
Mapigano makali yaripotiwa Omdurman, ndege ya abiria ya Uturuki yafyatuliwa risasi
Apr 28, 2023 07:58Mapigano yamezuka tena mepama leo katika mji mkuu wa Sudan, Khartoum, na milipuko imeendelea kusikika katika baadhi ya maeneo ya mji huo licha ya kuanza kutekelezwa kwa mapatano ya tano ya kusitisha vita tangu mapigano ya ndani yalipoanza kati ya Jeshi la Taifa na Vikosi vya Radiamali ya Haraka (RSF) nchini humo katikati ya mwezi huu.
-
Maelfu ya familia za Wasudani zakimbilia Misri wakihepa mapigano
Apr 28, 2023 03:47Maelfu ya wananchi wa Sudan wamevuka mpaka wa Arqin wa kaskazini mwa nchi hiyo na kuingia Misri wakikimbia mapigano yanayoendelea nchini kwao kati ya Jeshi la Taifa na vikosi vya jeshi la Radiamali ya Haraka (RSF) yaliyoanza katikati ya mwezi huu.
-
Vita Sudan: WHO yasema wagonjwa wengi hawawezi kupata huduma za afya
Apr 27, 2023 07:49Shirika la Afya Duniani WHO linasema mapigano nchini Sudan yamepelekea wagonjwa wengi wenye magonjwa sugu, kama vile ugonjwa wa figo, kisukari na saratani, kutoweza kufikia katika vituo vya afya au dawa wanazohitaji.
-
Upatanishi wa Wazayuni Sudan; kisingizio kingine cha kujipenyeza
Apr 26, 2023 07:28Katika hali ambayo mgogoro wa Sudan pamoja na vita vinaendelea kushuhudiwa, utawala haramu wa Israel umewaalika majerali mahasimu wa Sudan kwenda Tel Aviv kwa ajili ya upatanishi.
-
Jamii ya Kimataifa yatakiwa ichukue hatua kuepusha vita vya wenyewe kwa wenyewe Sudan
Apr 22, 2023 22:50Makundi ya Muungano wa Uhuru na Mabadiliko Sudan yametoa wito wa kuitaka Jamii ya Kimataifa ichukue hatua kuzuia kutokea vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo.
-
Jenerali Mkuu Sudan: Bado nina azma ya kukabidhi madaraka kwa serikali ya kiraia
Apr 21, 2023 22:07Jenerali Mkuu wa Sudan jana alieleza kuwa jeshi la nchi hiyo lingali lina nia ya kukabidhi madaraka kwa serikali ya kiraia. Hayo ni matamshi ya kwanza kutolewa kiongozi wa baraza la uongozi wa kijeshi la Sudan Jenerali Abdel Fattah al Burhan tangu kuanza karibu wiki moja iliyopita mapigano makali huko Sudan kati ya vikosi vitiifu kwa kiongozi huyo wa jeshi na askari kikosi cha radiamali ya haraka (RSF).
-
WHO yatahadharisha kuhusu hali mbaya ya kiafya nchini Sudan
Apr 21, 2023 03:52Msemaji wa Shirika la Afya Duniani (WHO) katika eneo la Mashariki ya Mediterania ametahadharisha kuhusu hali mbaya ya kiafya nchini Sudan kufuatia miapigano yanayoendelea baina ya makundi mawili ya jeshi la nchi hyo.
-
Maelfu wakimbia Sudan huku usitishaji mapigano ukigonga mwamba
Apr 20, 2023 08:55Maelfu ya wananchi wa Sudan wanakimbia mapigano yanayoendelea nchini humo leo yakiingia katika siku ya sita baada ya kugongwa mwamba jitihada za kusitisha mapigano. Hii ni mara ya pili ambapo usitishaji vita unakiukwa huko Sudan kati ya jeshi la taifana kundi lenye nguvu la wanajeshi wa Kikosi cha Radiamali ya Haraka (RSF).
-
Mapigano yameanza tena katika mji mkuu wa Sudan, Khartoum
Apr 19, 2023 03:30Ripoti za vyombo vya habari zinaeleza kuwa mapigano yamezuka upya kati ya vikosi vya jeshi la Sudan vinavyoongozwa na Jenerali Abdel-Fattah al-Barhan na vikosi vya Radiamali ya Haraka RSF vinavyoongozwa na Mohammed Hamdan Daghlo maarufu kama Hamidati katika mji mkuu wa nchi hiyo Khartoum.