-
Zaidi ya watu 180 wameuawa katika mapigano Sudan
Apr 18, 2023 03:35Takriban watu 185 wameuawa na wengine 1,800 kujeruhiwa katika mapigano ambaye yanaendelea kwa muda wa siku nne sasa kati ya pande zinazohasimiana nchini Sudan. Hayo ni kwa mujibu wa mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan huku jamii ya kimataifa ikitoa wito kwa pande hasimu kusitisha mapigano.
-
Umoja wa Afrika wakutana kuijadili Sudan;idadi ya vifo yakaribia 100
Apr 17, 2023 03:00Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika liliitisha kikao cha dharura jana kujadiliana hali ya kisiasa na usalama nchini Sudan.
-
Mapigano yaendelea nchini Sudan kwa siku ya tatu, kila upande unadai kudhibiti Ikulu ya Rais
Apr 16, 2023 22:44Mapigano makali yanaendelea katika mji mkuu wa Sudan, Khartoum, baada ya vita kuingia siku yake ya tatu, na zaidi ya watu 80 kuuliwa huku zaidi ya elfu moja wakijeruhiwa, kulingana na Shirika la Afya Duniani.
-
Juhudi za kufanya mapinduzi nchini Sudan
Apr 16, 2023 09:53Nchini Sudan hali si shwari ambapo habari kutoka nchini humo zinaonyesha kuendelea mapigano kati ya jeshi la Sudan na vikosi vya radiamali ya haraka na kuzusha wasiwasi wa kutokea mapinduzi katika nchi hiyo ya Kiafrika.
-
Mapigano ya kuwania madaraka baina ya majenerali yaingia siku ya pili nchini Sudan
Apr 16, 2023 06:56Mapigano kati ya jeshi la Sudan na Vikosi vya Radiamali ya Haraka yameingia siku ya pili, huku milipuko ikisikika tangu alfajiri ya leo, Jumapili, karibu na Mji wa Michezo, kusini mwa mji mkuu, Khartoum.
-
Madaktari Sudan: Zaidi ya watu 50 wameuawa, karibu 600 wamejeruhiwa katika mapigano
Apr 16, 2023 03:31Kamati Kuu ya Madaktari wa Sudan imetangaza kuwa takriban watu 56 wameuawa na wengine 595 wamejeruhiwa katika mapigano yanayoendelea nchini humo kati ya Jeshi na Kikosi cha Radiamali ya Haraka (RSF).
-
Sudan: Mapigano yazuka Khartoum kati ya jeshi la nchi na kikosi cha radiamalia ya haraka
Apr 15, 2023 08:05Milio ya risasi na milipuko imesikika katika mji mkuu wa Sudan, Khartoum, baada ya siku kadhaa za mvutano kati ya kikosi cha radiamali ya haraka na jeshi la nchi hiyo.
-
Al-Burhan na wapinzani wafichua sababu za kuchelewesha makubaliano ya mwisho ya amani
Apr 06, 2023 09:20Mkuu wa Baraza Kuu la Sudan, Abdel Fattah Al-Burhan, na wawakilishi wa mirengo mbalimbali ya kisiasa ya Sudan wamefichua sababu za kuchelewesha kutiwa saini makubaliano ya mwisho ya kisiasa, ambako kulipaswa kufanyika leo, Alhamisi.
-
Watu 14 waaga dunia baada ya mgodi kuporomoka Sudan
Apr 01, 2023 05:51Kwa akali watu 14 wamefariki dunia baada ya kuporomokewa na udongo kwenye mgodi wa dhahabu wa Jebel Al-Ahmar katika jimbo la Kaskazini nchini Sudan, mpakani na Misri.
-
Sudan kususia sarafu ya dola ya Marekani katika biashara na Russia
Mar 12, 2023 08:03Sudan inatafakari kusitisha matumizi ya sarafu ya dola ya Marekani katika miamala yake ya kibiashara na Russia.