-
Kujiondoa kwa Baraza la Kijeshi la Sudan katika mchakato wa mazungumzo na makundi ya kisiasa
Jul 05, 2022 21:56Kamanda Mkuu wa Jeshi la Sudan ametangaza kujiondoa kwa Baraza la Kijeshi la nchi hii katika mazungumzo ya moja kwa moja na makundi ya kisiasa.
-
Tisa wauawa Sudan katika maandamano ya kupinga utawala wa kijeshi
Jul 01, 2022 05:56Takriban waandamanaji tisa waliuawa kwa kupigwa risasi nchini Sudan siku ya Alhamisi, matabibu wamesema, huku umati mkubwa wa watu ukiingia mitaani licha ya ulinzi mkali na kukatika kwa mawasiliano kuandamana dhidi ya utawala wa kijeshi ulionyakua mamlaka miezi minane iliyopita.
-
AU yataka Sudan, Ethiopia ziache makabiliano ya kijeshi mpakani
Jun 30, 2022 03:42Kamisheni ya Umoja wa Afrika imetoa mwito kwa nchi za Sudan na Ethiopia kujizuia na kutochukua hatua yoyote inayoweza kushadidisha mivutano ya kijeshi katika eneo la al-Fashaqa, lililoko katika mpaka wa pamoja wa nchi mbili hizo jirani.
-
Khartoum yaituhumu Addis Ababa kuwanyonga wafungwa wa Sudan na kuonyesha miili yao
Jun 27, 2022 22:21Jeshi la Sudan limelitumu jeshi la Ethiopia kuwa limewanyonga wanajeshi 7 na raia mmoja wa Sudan waliokuwa wafungwa nchini humo, jambo ambalo limekanushwa na maafisa rasmi wa Ethiopia, wakieleza kuwa Addis Ababa itatoa tamko rasmi la kujibu madai hayo ya Sudan.
-
Mvutano baina ya Ethiopia na Sudan: Jeshi la Ethiopia latuhumiwa kuwaua Wasudan wanane
Jun 27, 2022 03:26Sudan imesema, jeshi la Ethiopia limeua raia wanane wa nchi hiyo.
-
UN: Thuluthi moja ya Wasudan wanakabiliwa na njaa
Jun 17, 2022 06:52Mashirika ya Umoja wa Mataifa yamesema zaidi ya asilimia 30 ya wananchi wa Sudan wanasumbuliwa na mgogoro mkubwa wa chakula uliosababishwa na mabadiliko ya tabianchi, mzozo wa kisiasa na kupanda bei za chakula katika soko la dunia.
-
UN: Mauaji mapya ya kikabila nchini Sudan yameua watu 145
Jun 15, 2022 07:19Umoja wa Mataifa umesema idadi ya watu waliouawa katika wimbi jipya la mapigano ya kikabila huko Sudan imeongezeka na kufikia 145.
-
Idadi ya watu waliouawa katika mapigano ya kikabila Sudan yafikia 100
Jun 13, 2022 03:28Imeelezwa kuwa, idadi ya watu waliouawa katika mapigano ya kikabila ya hivi karibuni huko Darfur magharibi Sudan imeongezeka na kufikia wahanga 100.
-
Watu wasiopungua 27 wauawa katika mapigano ya kikabila nchini Sudan
Jun 07, 2022 23:09Watu wasiopungua 27 wameuawa na makumi ya wengine wamejeruhiwa katika mapigano yaliyotokea kwenye maeneo ya magharibi na kusini ya Sudan.
-
Mtaalamu wa UN ataka kuharakishwa uchunguzi wa mauaji ya baada ya mapinduzi ya kijeshi Sudan
Jun 05, 2022 03:36Mtaalamu wa Umoja wa Mataifa wa haki za binadamu nchini Sudan ametaka kuharakishwa uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji pamoja na jinai zingine zilizofanywa katika nchi hiyo, huku idadi ya vifo vilivyotokea tangu yalipofanyika mapinduzi ya kijeshi mwaka uliopita ikikaribia watu 100.