-
Tanzania yapata nafasi muhimu ya sayansi na teknolojia Umoja wa Mataifa
Jan 18, 2022 23:27Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Kiuchumi na Kijamii, ECOSOC, Collen Vixen Kelapile ameiteua nchi ya Tanzania kuwa Mwenyekiti Mwenza wa Jukwaa la Saba la Wadau Mbalimbali wa Masuala ya Sayansi, Teknolojia na Uvumbuzi katika kutekeleza Agenda ya 2030 ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa, SDGs.
-
Athari za mabadiliko ya tabianchi; kiangazi chaua mifugo 62,000 Tanzania
Jan 15, 2022 08:43Kipindi kirefu cha kiangazi kimeua makumi ya maelfu ya mifugo katika wilaya ya Simanjiro mkoani Manyarahuku, kaskazini mwa Tanzania, huku makali ya ukame yakiendelea kushuhudiwa katika pembe mbalimbali za dunia.
-
Ajali ya gari la waandishi habari yaua watu wasiopungua 14 Simiyu, Tanzania
Jan 11, 2022 10:43Watu wasiopungua 14 wamefariki dunia baada ya gari ya waandishi wa habari iliyokuwa kwenye msafara wa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza (RC), Robert Gabriel kugongana na gari ya abiria aina ya Toyota Hiace katika eneo la Nyamikoma wilaya ya Busega Mkoani Simiyu.
-
Biashara ya Kenya na Tanzania yaimarika kufuatia agizo la Rais Samia
Jan 09, 2022 04:34Biashara baina ya Kenya na Tanzania inazidi kuimarika miezi kadhaa baada ya kuja madarakani Rais Samia Suluhu Hassan nchini Tanzania.
-
Job Yustino Ndugai, Spika wa Bunge la Tanzania ajiuzulu
Jan 06, 2022 10:45Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Job Ndugai ametangaza kujiuzulu wadhifa wake huo ndani ya Bunge leo Alkhamisi, Januri 6, 2022.
-
Watu 9 waaga dunia kwa kuzama baharini kisiwani Pemba, wengine hawajulikani waliko
Jan 04, 2022 23:50Watu tisa wamefariki dunia na wengine kadhaa kuokolewa baada ya boti waliokuwa wakisafiria kuzama Mkoa wa Kusini Pemba.
-
Serikali ya Tanzania yawataka raia wachukue tahadhari ya magonjwa ya kuambukiza
Dec 18, 2021 04:44Wizara ya Afya ya Tanzania imewataka raia kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya magonjwa ya kuambukiza, wakati huu hospitali nyingi nchini humo, zikiripoti ongezeko la wagonjwa wanaougua mafua, kifua na maumivu ya viungo.
-
Mkuu wa Kanisa la Kilutheri Tanzania aomba Wimbo wa Taifa ubadilishwe
Dec 07, 2021 12:27Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Askofu Fredrick Shoo, ameomba neno HAKI liongezwe katika wimbo wa taifa hilo, akisisitiza kuwa ni tunda la amani ya nchi.
-
Sisitizo la Rais wa Tanzania kwa mkutano wa COP26: Tunapimwa kwa vitendo vyetu, si kwa ahadi kubwa kubwa tunazotoa
Nov 02, 2021 04:09Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewaeleza viongozi wa mataifa ya dunia wanaohudhuria mkutano wa 26 wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi COP26 huko Glasgow, Scotland, kwamba mshikamano na juhudi zao kama viongozi katika kukabili mabadiliko ya tabianchi vitapimwa si kwa ahadi kubwa wanazotoa kwenye mkutano huo bali kwa jinsi watakavyotekeleza vipengele vyote vya mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi.
-
Rais wa Tanzania: Tutaendelea Kushirikiana na Burundi
Oct 22, 2021 11:13Tanzania imesema itaendelea kushirikiana na Burundi katika kuimarisha ulinzi katika mipaka ya nchi hizo mbili. Hayo yamesemwa na Rais Samia Suluhu Hassan wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika mazungumzo yake huko Chamwino Dodoma na Rais wa Burundi, Évariste Ndayishimiye ambaye yupo nchini humo kwa ziara ya siku tatu.