-
Hatimaye Erick Kabendera aachiliwa huru baada ya kukiri makosa na kulipa sehemu ya faini
Feb 24, 2020 10:29Hatimaye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ya jijini Dar es salaam imemwachilia huru mwandishi wa habari za uchunguzi, Erick Kabendera na kumwamuru alipe faini na fidia ya jumla ya Shilingi milioni 273 baada ya kukiri makosa yaliyokuwa yanamkabili yakiwemo ya utakatishaji fedha na ukwepaji kodi huku akiondolewa shitaka la kuongoza genge la uhalifu.
-
Kambi ya upinzani Tanzania yapata pigo jingine baada ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chadema kutimkia CCM
Feb 18, 2020 13:12Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama kikuu cha upinzani cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) nchini Tanzania Dk Vicent Mashinji leo Jumanne Februari 18 amehamia chama tawala CCM na kupokewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Humphrey Polepole.
-
Balozi Kairuki: Serikali Haitawarudisha Tanzania wanafunzi walioko China + Sauti
Feb 12, 2020 09:20Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa Kairuki amesema wanafunzi wanaosoma katika mji wa Wuhan hawawezi kurudi kwa sababu kuna katazo la kutoingia wala kutoka kwenye mji huo kutokana na maambukizi ya virusi vya corona.
-
Rais wa Tanzania amfuta kazi afisa wa serikali aliyeichana Qurani
Feb 11, 2020 09:24Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli amemuagiza Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo, kuhakikisha anamuandikia barua ya kumfukuza kazi mfanyakazi wa wizara hiyo aliyechana na kuitemea mate Qurani Takatifu mkoani Morogoro.
-
Membe: Nimefurahi sana kuhojiwa na Kamati ya CCM, sehemu ya niliyoulizwa itakuwa ikitoka kidogokidogo
Feb 06, 2020 12:42Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje nchini Tanzania, Bernard Membe amesema kuwa safari yake ya kwenda Dodoma ilikuwa ya manufaa makubwa sana kwake, kwa chama cha Mapinduzi CCM na kwa Taifa na kwamba masuala mengine aliyohojiwa na kamati ya chama hicho yataendelea kutoka kidogokidogo hapo baadaye.
-
Wanajeshi 10 wa Tanzania wapoteza maisha wakati wakifanya mazoezi
Feb 03, 2020 10:39Jeshi la Ulinzi la Tanzania limetangaza kuwa askari 10 wa jeshi hilo wamepoteza maisha wakati wakifanya mazoezi.
-
Radiamali za nchi zilizowekewa vikwazo vya usafiri na Marekani
Feb 02, 2020 04:04Serikali ya Eritrea imekosoa vikali hatua ya Washington ya kuwawekea vizingiti raia wa nchi hiyo ya Pembe ya Afrika wanaotaka kwenda Marekani ikisisitiza kuwa, vikwazo hivyo vya usafiri havikubaliki.
-
Makumi wapoteza maisha wakigombania 'mafuta ya upako' Tanzania + Sauti
Feb 02, 2020 00:13Kwa akali watu 20 wameaga dunia katika mkanyagano wa harakati za kutaka kukanyaga 'mafuta ya upako' kwenye kongamano la 'Mtume' Boniface Mwaiposa lililofanyika uwanja wa Majengo mjini Moshi mkoani Kilimanjaro, kaskazini mashariki mwa Tanzania jioni ya jana Jumamosi.
-
Baada ya Lugola kupigwa kalamu nyekundu, Rais Magufuli amemteua Simbachawene kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani wa Tanzania
Jan 23, 2020 12:30Rais John Pombe Magufuli wa Tanzania amemteua George Simbachawene kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, nafasi iliyokuwa ikishikiliwa na Kangi Lugola mbunge wa Mwibara (CCM). Hayo yameelezwa jioni ya leo na katibu mkuu kiongozi, Balozi John Kijazi.
-
Tanzania, Nigeria katika nchi zitakazowekewa vikwazo vya usafiri na Marekani
Jan 22, 2020 08:37Marekani ina mpango wa kuziongeza nchi nyingine saba zikiwemo Tanzania na Nigeria kwenye orodha ya nchi ambazo raia wake wanatarajiwa kuwekewa vikwazo na vizingiti vya kuingia nchini humo.