-
Polisi Tanzania: Hatujabaini silaha iliyotumika kumuua Akwilina, Lema ashangaa
Mar 31, 2018 00:07Kamanda wa jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es Salaam nchini Tanzania, Lazaro Mambosasa, amesema kuwa hadi sasa bado jeshi hilo linaendelea na uchunguzi kuhusu tukio la kuuawa kwa kupigwa risasi mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwilini.
-
Viongozi wa CHADEMA kulala mahabusu hadi Aprili 3; hakimu adai masharti ya dhamana hayajakamilika
Mar 29, 2018 11:12Vyombo vya habari nchini Tanzania vimeripoti kuwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeamuru Viongozi 6 wa CHADEMA akiwemo mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe, wafikishwe mahakamani hapo AprilI 3, 2018 ili kukamilisha masharti ya dhamana yao.
-
Tundu Lissu: Kinachowapata viongozi wa upinzani Tanzania, ni njia ya kuelekea Ikulu
Mar 29, 2018 00:10Mbunge wa Singida Mashariki na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) nchini Tanzania, Tundu Lissu amesema kuwa, kile kinachowapata viongozi wa chama kikuu cha upinzani cha Demokrasia na Maendelea (CHADEMA), ni maandalizi ya upinzani huo kuingia madarakani.
-
Viongozi wa upinzani Tanzania wakamatwa; wapandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka
Mar 27, 2018 12:53Viongozi kadhaa wa chama cha upinzani cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) nchini Tanzania wamepandishwa kizimbani mchana wa leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam na kusomewa mashtaka manane yakiwemo ya kufanya maandamano yaliyosababisha kifo cha Mwanafunzi wa Chuo cha NIT, Akwilina Akwiline, uasi, kuhamasisha chuki kati ya wanajamii na kuchochea ghasia.
-
Magufuli awajibu maaskofu, awataka wahubiri viwanda na si mambo mengine
Mar 26, 2018 10:41Rais John Magufuli wa Tanzania amejibu mapigo ya maaskofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT) akiwataka viongozi hao wahubiri kuhusu ujenzi wa viwanda vya dawa nchini humo ili Tanzania isinunue dawa nje ya nchi, badala ya kuhubiri mambo mengine.
-
Hatimaye Abdul Nondo aachiliwa huru na mahakama ya Tanzania kwa dhamana
Mar 26, 2018 04:17Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Iringa Jumatatu ya leo, imemuachilia huru Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi nchini Tanzania (TSNP), Abdul Nondo kwa dhamana.
-
Ghasia zaibuka Mbeya, Tanzania baada ya polisi kutuhumiwa kusababisha mauaji ya kijana mmoja
Mar 26, 2018 03:29Ghasia na machafuko yameripotiwa kutokea mkoani Mbeya, kusini magharibi mwa Tanzania baada ya polisi kutuhumiwa kuwa wamesababisha kifo cha kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la Allen Mapunda, mkazi wa Kata ya Iyela.
-
Rais Magufuli, aomboleza vifo vya watu 26 katika ajali ya gari mkoani Pwani Tanzania
Mar 25, 2018 09:59Rais John Pombe Magufuli wa Tanzania, ametuma salamu za rambirambi kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Evarist Ndikilo na familia za wahanga wa ajali ya basi ndogo aina ya Hiace iliyosababisha vifo vya watu 26 na wengine kadhaa kujeruhiwa.
-
Maalim Seif amuonya Profesa Lipumba amtaka aache kukivuruga chama cha CUF Tanzania
Mar 24, 2018 12:15Katibu Mkuu wa Chama Cha Wanachi (CUF), Maalif Seif Sharif Hamad, amemkemea mwenyekiti wa chama hicho anayetambuliwa na msajili wa vyama vya siasa nchini Tanzania, Profesa Ibrahimu Haruna Lipumba na kumtaka kuacha kukivuruga chama hicho.
-
Hatimaye Abdul Nondo amefikishwa Mahakamani Iringa Tanzania
Mar 21, 2018 04:52Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo amesafirishwa usiku wa kuamkia leo Machi 21, 2018 kupelekwa mkoani Iringa.