-
Machafuko yaendelea Tunisia, jeshi kumiminwa mitaani kuwasaidia polisi
Jan 19, 2021 03:14Vijana wenye hasira wameendelea kukaidi amri ya karantini ya nchi nzima huko Tunisia hasa nyakati za usiku na wameendelea kufanya maandamano licha ya kuweko maambukizi ya kirusi cha corona.
-
Makumi ya wahajiri wafa maji katika pwani ya Tunisia
Dec 25, 2020 13:05Wahajiri wasiopungua 20 wamepoteza maisha katika ajali ya boti iliyotokea jana Alkhamisi katika mji wa pwani wa Sfax nchini Tunisia.
-
Algeria na Tunisia zazuia ndege ya Israel kutumia anga zao
Dec 23, 2020 12:26Algeria na Tunisia zimeizuia ndege ya utawala wa Kizayuni wa Israel kuruka katika anga zao ili kuonyesha upinzani wao kwa hatua ya baadhi ya nchi za Kiarabu ya kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala huo haramu.
-
Wizara ya Mashauri ya Kigeni: Tunisia haina mpango wa kuanzisha uhusiano wa kawaida na Israel
Dec 23, 2020 08:05Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Tunisia imeashiria juhudi za baadhi ya mataifa ya kieneo za kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala haramu wa Israel na kusisitiza kwamba, serikali ya Tunis haina mpango wa kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala huo ghasibu.
-
Vyama na shakhsia wa Tunisia walaani kuuliwa kigaidi Shahidi Fakhrizadeh
Dec 01, 2020 04:32Vyama na shakhsia mbalimbali nchini Tunisia wametoa taarifa na kulaani mauaji ya kigaidi ya Shahidi Mohsen Fakhrizadeh, mwanasayansi mkubwa wa nyuklia na masuala ya ulinzi wa Iran.
-
Mkuu wa Harakati ya An Nahdhah nchini Tunisia ajiengua kugombea nafasi ya mkuu wa chama
Nov 26, 2020 04:36Mkuu wa Harakati ya An Nahadhah ya nchini Tunisia amesema hatagombea nafasi ya mkuu wa harakati hiyo kwa duru ya tatu mtawalia.
-
Moncef Marzouki: Tawala za Kiarabu hazijaanzisha uhusiano na Israel bali 'zimejisalimisha'
Nov 21, 2020 08:02Mohamed Moncef Marzouki, rais wa zamani wa Tunisia amesema kuwa, ni kosa kusema kuwa, baadhi ya nchi za Kiarabu zimeanzisha uhusiano wa kawaida na utawala haramu wa Israel, bali lililo sahihi na ambalo ndio ukweli wa mambo ni kuwa, mataifa hayo yamejisalimisha kwa utawala huo vamizi.
-
Rais wa zamani wa Tunisia aikosoa vikali Jumuiya ya Nchi za Kiarabu
Nov 07, 2020 10:34Rais wa zamani wa Tunisia Muhammad Moncef al-Marzouki amekosoa vikali kimya cha Jumuiya ya Nchi za Kiarabu (Arab League) na kutolaani kwake mwenendo wa baadhi ya nchi za jumuiya hiyo wa kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala haramu wa Israel.
-
Sudan yakanusha kuanzisha uhusiano na utawala wa Kizayuni
Oct 16, 2020 02:39Duru moja ya kuaminika ndani ya Baraza la Uongozi la Sudan imekanusha taarifa zinazodai kuwa kumefikiwa makubaliano ya kuanzishwa uhusiano wa kawaida baina ya baraza hilo na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Mamia wapambana na polisi Tunisia baada ya muuza sigara kuuawa kwa buldoza
Oct 14, 2020 02:23Mamia ya waandamanaji waliokuwa wakirusha mawe walipambana na polisi katika mji wa Sbeitla nchini Tunisia jana Jumanne baada ya mamlaka kushambulia kibanda cha sigara ambacho hakina leseni, na kumuua mmiliki wake aliyekuwa amelala ndani yake.