-
Iran yakosoa undumakuwili wa Ufaransa juu ya suala la haki za binadamu
Mar 12, 2023 04:29Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani undumakuwili wa Ufaransa, ambayo kwa upande mmoja inajinadi kuwa mbeba bendera ya kutetea haki za binadamu, lakini kwa upande wa mwngine inakanyaga haki hizo kwa vitendo.
-
Waziri Mkuu wa Mali: Tuna ushahidi, Ufaransa inashirikiana na magaidi
Mar 08, 2023 03:07Waziri Mkuu wa Mali, Choguel Kokalla Maïga, amefichua - katika mahojiano maalumu na televisheni ya Al-Jazeera ya Qatar- kuwa Bamako ina taarifa sahihi na ushahidi kwamba baadhi ya magaidi waliko nchini Mali wamekuwa wakiwasiliana na Ufaransa.
-
Burkina Faso yavunja rasmi makubaliano ya kijeshi ya 1961 na Ufaransa
Mar 02, 2023 09:39Burkina Faso imevunja rasmi makubaliano ya kijeshi iliyosaini na Ufaransa mwaka 1961, wiki chache baada ya kumtaka mkoloni wake huyo wa zamani kuondoa vikosi vyake na balozi wake nchini humo.
-
Kuondoka vikosi vya Ufaransa katika nchi ya Burkina Faso
Feb 21, 2023 07:22Hatimaye vikosi vya Ufaransa vimeondoka nchini Burkina Faso na kuhitimisha uwepo wake katika nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika uliodumu kwa miaka 10.
-
Baada ya kutimuliwa Ufaransa, magaidi 160 waangamizwa Burkina Faso
Feb 21, 2023 04:01Magaidi wasipoungua 160 wameangamizwa katika operesheni ya jeshi la Burkina Faso katika eneo la Sahel, wakati huu ambapo mabaki ya askari vamizi wa Ufaransa wanaendelea kuondoka nchini humo.
-
Iran yamshambulia Macron kwa kukutana na wanaopinga Mapinduzi ya Kiislamu
Feb 18, 2023 06:49Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amemjia juu Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa kwa kukutana na 'shakhsia' wanaopinga mfumo wa uongozi na Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran tokeo mwaka 1979.
-
Polisi ya Ufaransa yakandamiza maandamano ya wananchi
Feb 12, 2023 23:04Askari polisi nchini Ufaransa wamewashambulia vibaya mamia ya maelfu ya watu walioshiriki maandamano ya kulalamikia sera za Rais Emmanuel Macron wa nchi hiyo, na hususan mageuzi tata ya pensheni yaliyotazamiwa kuanza kutekelezwa mwaka huu wa 2023.
-
Tathmini ya maandamano ya ‘watu mamilioni moja’ Ufaransa ya kupinga sera za serikali ya Macron
Feb 12, 2023 23:03Takribani watu milioni moja waliandamana siku ya Jumamosi nchini Ufaransa ikiwa ni mara ya nne wakipinga sera za serikali ya Rais Emmanuel Macron.
-
Iran yajibu uropokaji wa Macron, yamtaka azungumzie silaha za nyuklia za Israel
Feb 03, 2023 23:55Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amekosoa matamshi ghalati ya Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa aliyedai katika mazungumzo yake na Benjamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa utawala haramu wa Israel kuwa, eti Paris inatiwa wasiwasi na shughuli za nyuklia za Jamhuri ya Kiislamu.
-
Waziri: Migomo itatatiza usafiri wa umma kote nchini Ufaransa
Jan 29, 2023 23:16Waziri wa Uchukuzi wa Ufaransa amesema migomo ya wafanyakazi wa sekta hiyo kuanzia kesho Jumanne inatazamiwa kulemaza usafiri wa umma katika pembe zote za nchi hiyo ya Ulaya.