-
Kuingia vita vya Ukraine katika hatua mpya na kuzidisha mzozo kati ya Russia na NATO
Nov 23, 2024 22:56Matukio ya hivi karibuni katika vita vya Ukraine, yaani uamuzi wa nchi za Magharibi wa kutoa ruhusa kwa Ukraine kuishambulia Russia kwa kutumia silaha za masafa marefu za Marekani na Ulaya kwa upande mmoja, na Russia kutumia w kombora jipya la masafa ya kati lenye kasi ya zaidi ya sauti dhidi ya Ukraine kama tahadhari kali kwa Magharibi, kumeibua mgogoro mkubwa na usio na kifani kati ya Russia na NATO.
-
Hatua mpya ya Wamagharibi ya kuchochea moto wa vita vya Ukraine
Nov 18, 2024 07:43Rais wa Marekani, Joe Biden ameripotiwa kuidhinisha Ukraine kutumia makombora ya masafa marefu ya Kimarekani kulenga shabaha ndani ya mipaka ya Russia ya kabla ya 2014. Hayo ni kwa mujibu wa ripoti ya jana Jumapili iliyotolewa na gazeti la New York Times likiwanukuu maafisa wa Marekani ambao hawakutaka kutajwa majina yao.
-
Russia yaitahadharisha Ufaransa kuhusu kutuma makombora Ukraine
Nov 15, 2024 00:24Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia ametahadharisha kuhusu Ufaransa kutuma makombora nchini Ukraine.
-
Ufaransa yamkamata mwanaharakati anayepinga ukoloni Afrika
Oct 16, 2024 03:39Mwanaharakati na mwanamajimui mashuhuri wa kupinga ukoloni mamboleo barani Afrika, Stellio Gilles Robert Capo Chichi, maarufu kama Kemi Seba, amekamatwa nchini Ufaransa.
-
Waziri Mkuu wa zamani wa Ufaransa: Hali ya mambo ya Gaza ni kashfa kubwa zaidi ya kihistoria
Sep 14, 2024 01:08Waziri Mkuu wa zamani wa Ufaransa ametaja hali ya mambo huko Gaza kuwa ni "kashfa kubwa zaidi ya kihistoria" na kukosoa msimamo wa Ufaransa kuhusu vita vinavyoendelea katika eneo hilo.
-
Mali yaendelea 'kuviadhibu' vyombo vya habari vya Ufaransa
Sep 12, 2024 08:07Serikali ya kijeshi ya Mali imepiga marufuku kanali nyingine ya televisheni ya Ufaransa kurusha matangazo yake kwa kukiuka Sheria ya Kudhibiti Vyombo vya Habari katika nchi hiyo ya Afrika Magharibi.
-
Mali yasimamisha matangazo ya televisheni ya LCI ya Ufaransa kwa upotoshaji
Aug 25, 2024 11:29Serikali ya kijeshi ya Mali imepiga marufuku kanali ya televisheni ya Ufaransa ya LCI kurusha matangazo yake kwa muda wa miezi miwili kutokana na kile kilichotajwa kuwa upotoshaji kuhusu hali ya usalama wa nchi hiyo ya Afrika Magharibi.
-
Rais Pezeshkian aonya: Matokeo hasi 'mazito' yanaingojea Israel ikijaribu kuishambulia Lebanon
Jul 29, 2024 23:47Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameonya kuwa matokeo hasi 'mazito' utayapata utawala wa Kizayuni wa Israel ikiwa utafanya kosa kubwa la kushambulia kijeshi Lebanon.
-
Uturuki: Netanyahu mfanya mauaji ya kimbari atakuwa na mwisho kama wa Hitler
Jul 29, 2024 02:32Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki imesema: "kama ulivyokuwa mwisho wa mfanya mauaji ya kimbari Hitler, ndivyo pia utakavyokuwa mwisho wa mfanya mauaji ya kimbari Netanyahu."
-
Rais wa DRC amkosoa mwenzake wa Kenya kwa 'kuushughulikia vibaya' Mchakato wa Nairobi
Jul 27, 2024 08:04Rais Félix Tshisekedi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) amemkosoa mwenzake wa Kenya William Ruto kwa alichokiita kushughulikia vibaya Mchakato wa Nairobi, ambao ulibuniwa kuanzisha mazungumzo na makundi yenye silaha mashariki mwa DRC. Tshisekedi amemshutumu Ruto kuwa anaegemea upande wa Rwanda, msimamo anaoamini umekwamisha mpango huo.