-
Vyama 20 vyalitaka Baraza la Kijeshi linalotawala Mali kutupilia mbali mpango wa kuondoa dini katika rasimu ya katiba
May 07, 2023 11:01Takriban vyama 20 nchini Mali vimeunganisha pamoja juhudi zao na kulitaka baraza tawala la kijeshi kufuta kipengee kwenye rasimu ya katiba mpya kinachosisitiza kuwa serikali ya nchi hiyo itakuwa ya kilaiki. Rasimu hiyo imepangwa kupigwa kura ya maoni mwezi ujao wa Juni.
-
Kiongozi wa Waislamu Canada: Waislamu kote nchini wana sababu ya kuwa na wasiwasi baada ya hujuma ya msikiti wa Ontario
Apr 12, 2023 02:12Kiongozi wa Jumuiya ya Waislamu nchini Canada ameeleza wasiwasi wake kuhusu kushamiri vetendo vya chuki dhidi ya Uislamu nchini humo baada ya mwanamume mmoja kuvamia msikiti wa jimbo la Ontario Alhamisi iliyopita, kutoa vitisho sambamba na kujaribu kuwavamia waumini nje ya msikiti huo.
-
Aliachwa akihangaika na kifo peke yake; Hasira zatanda Ufaransa baada ya kifo cha mwanafunzi mwenye asili ya Kiarabu
Mar 25, 2023 02:20Mitandao ya kijamii nchini Ufaransa imeshuhudia wimbi kubwa la hasira na ghadhabu baada ya kifo cha mwanafunzi mwenye asili ya Kiarabu ambaye alipatwa na mshtuko wa moyo, huku kukiwa na shutuma kwamba uongozi wa shule ulimwacha akikabilina na kifo peke yake bila ya kumpa huduma ya dharura.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Pakistan: Uislamu ni mlindaji mkubwa zaidi wa haki za wanawake
Mar 09, 2023 07:07Waziri wa Mambo ya Nje wa Pakistan amesema, Uislamu ni mlindaji mkubwa zaidi wa haki za wanawake.
-
Waislamu waadhimisha kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa Imam Ali bin Abi Twalib (AS)
Feb 04, 2023 07:41Iran imejiunga na uliwengu wa Kiislamu hii leo katika kuadhimisha siku ya kukumbuka kuzaliwa Amirul Muumin Ali (A.S) Imam wa Kwanza wa Waislamu wa Kishia ulimwenguni.
-
Warepublican waanza mchakato wa kumuondoa Ilhan Omar katika Kamati ya Mambo ya Nje ya Congresi kwa kuikosoa Israel
Feb 02, 2023 12:11Wanachama wa Republican katika Baraza la Wawakilishi la Marekani wanajiandaa kupigia kura muswada wa kumuondoa mwakilishi wa Kidemokrati, Ilhan Omar kwenye Kamati ya Masuala ya Kigeni, siku chache baada ya kuondolewa katika Kamati ya Masuala ya Afrika, kutokana na kukosoa ukatili na mauaji yanayofanywa na Israel dhidi ya raia wa Palestina.
-
Twitter ya Elon Musk yawakasirisha Waislamu Marekani, "CAIR" yamtaka ajifunze Uislamu
Jan 01, 2023 04:14Bilionea wa Kimarekani, Elon Musk, ambaye ni mmiliki wa mtandao wa kijamii wa Twitter, amewakasirisha Waislamu nchini Marekani baada ya kuchapisha picha kwenye akaunti yake ya Twitter, ikiwa na idadi ya alama za fikra na itikadi anazodai zinalenga "kupindua na kuharibu fikra na akili za watu."
-
Rais wa Iran amtumia Papa Francis Salamu za Krismasi
Dec 26, 2022 12:01Rais Sayyid Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametuma salamu za pongezi kwa mnasaba wa siku ya kuzaliwa Nabii Isa bin Maryam-Amani ya Mwenyezi Mungu Iwe Juu Yake-na kuwadia mwaka mpya wa Miladia.
-
Mkutano wa kimataifa wa mazungumzo ya Uislamu na Uhindu mjini New Delhi India
Dec 13, 2022 11:50Duru ya tatu ya mkutano wa kimataifa wa mazungumzo ya Uislamu na Uhindu iliyokuwa na anuani ya "Mchango wa Dini wa Kuishi Pamoja Katika Amani na Ustawi" umefanyika mjini New Delhi kwa kuhudhuriwa na makhatibu, shakhsia wenye vipawa na Maulamaa wa Iran na India.
-
Licha ya kufungwa misikiti 24 nchini Ufaransa, Marine Le Pen ataka misikiti zaidi ifungwe
Oct 05, 2022 07:09Mwanasiasa mwenye siasa kali za mrengo wa kulia wa Ufaransa, Marine Le Pen amemtaka Waziri wa Mambo ya Ndani wa nchi hiyo, Gérald Darmanin, kufunga misikiti zaidi ya Waislamu akisema kuwa kufungwa misikiti 24 katika kipindi cha miaka miwili iliyopita haitoshi.