-
Qassemi: Hakuna imani yoyote ya kufanya mazungumzo na Marekani
Aug 07, 2018 10:08Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuhusu matamshi ya karibuni ya rais wa Marekani kuwa yuko tayari kufanya mazungumzo na viongozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, kwamba: kutokana na sera za Marekani za kuendesha vita vikubwa vya kisaikolojia dhidi ya Iran hakuna dhamana wala imani yoyote juu ya serikali ya Marekani wala rais wa nchi hiyo.
-
Mashauriano ya Lavrov na Merkel kuhusu Syria
Jul 25, 2018 22:33Tangu mwezi Disemba mwaka 2015 Russia ilituma majeshi katika nchi ya Syria kwa ajili ya kupambana na makundi ya kigaidi na vilevile kuisaidia serikali halali ya nchi hiyo.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani: Marekani haiaminiki tena
Jul 16, 2018 22:24Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Ujerumani amejibu matamshi na hujuma ya maneno ya Rais wa Marekani aliyeutaja Umoja wa Ulaya kuwa ni "adui" kwa kusema: Ulaya haiwezi tena kuitegemea Ikulu ya Rais wa Marekani.
-
Trump aibua mifarakano katika muungano wa kijeshi wa NATO
Jul 12, 2018 05:03Siku ya kwanza ya kikao cha viongozi wa muungano wa kijeshi wa nchi za Magharibi, NATO, imemalizika huku mkutano huo ukishuhudia mashambulizi makali ya maneno ambayo hayajawahi kushuhudiwa ya Rais Donald Trump wa Marekani dhidi ya Ujerumani, moja kati ya nchi muhimu zaidi katika muungano huo wa NATO.
-
Dakta Kharrazi: Vitendo vya kibabe vya Marekani vimesababisha ukosefu wa usalama Mashariki ya Kati
Jul 11, 2018 03:43Mkuu wa Baraza la Kistratijia la Uhusiano wa Nje wa Iran amesema kuwa, uingiliaji wa madola ya kigeni katika masuala ya ndani ya nchi nyingine na miamala ya kibabe ya Marekani na utawala haramu wa Israel kuhusiana na Wapalestina ni mambo muhimu ambayo yamechangia mno kukosekana amani na uthabiti katika eneo la magharibi mwa Asia (Mashariki ya Kati)
-
Misri: Migogoro ya kieneo haiwezi kupatiwa ufumbuzi kwa mtutu wa bunduki
Jul 05, 2018 03:03Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Misri amesema kuwa, nchi yake inafanya juhudi kubwa katika mwenendo wa kupatiwa ufumbuzi migogoro wa Syria na Libya na kusisitiza kwamba, migogoro inayoshuhudiwa hivi sasa katika eneo la Mashariki ya Kati na kaskazini mwa Afrika ufumbuzi wake sio mtutu wa bunduki.
-
Magazeti ya Ujerumani yamkosoa Trump, yamwita "mpumbavu"
Jun 12, 2018 03:47Magazeti ya Ujerumani yamemtaja Rais Donald Trump wa Marekani kuwa ni mtu asiyejua mipaka yake wala asiye na mantiki na yamezitaka nchi zote za Ulaya kuacha kumfuata kiongozi huyo.
-
Wanasiasa wa Ujerumani wamjia juu balozi wa Marekani kwa kuingilia biashara za Berlin na Iran
Jun 05, 2018 22:03Wanasiasa nchini Ujerumani wamemjia juu balozi wa Marekani mjini Berlin kwa matamshi yake ya kijuba yaliyo dhidi ya mashirika ya Ujerumani yanayoendesha shughuli zao nchini Iran.
-
Ujerumani yaipigia magoti Iran, yaitaka isijiondoe JCPOA
May 29, 2018 23:17Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani amesema Berlin iko tayari kuimarisha uhusiano wa kiuchumi na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran madhali Tehran itaendelea kufungamana na mapatano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Kansela wa Ujerumani Merkel apoteza matumaini kuhusu Marekani
May 11, 2018 03:44Kansela Angela Merkel wa Ujerumani kwa mara nyingine amesema nchi za Ulaya haziwezi kuendelea kuitegemea Marekani katika masuala ya kijeshi na kujihami. Merkel amewataka waitifaki wa Ujerumani barani Ulaya wachukue hatima ya bara hilo mikononi mwao kwani Marekani haiwezi kutegemewa tena.