-
Wazayuni waendelea kufanya mauaji ya kinyama Ghaza, kutokea angani, ardhini na baharini
Dec 30, 2023 23:00Mashambulizi ya kinyama na kikatili ya utawala wa Kizayuni ya angani, ardhi na majini yanaendelea kwenye Ukanda wa Ghaza hasa katika maeneo ya katikati na kusini mwa ukanda huo.
-
WHO: Dunia ichukue hatua za dharura kuzuia maafa zaidi Gaza
Dec 28, 2023 03:09Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa mara nyingine tena limeeleza wasi wasi wake kuhusu hali ya kutisha ya kibinadamu katika Ukanda wa Gaza na kusisitiza kuwa, jamii ya kimataifa ina wajibu wa kuchukua hatua za dharura za kukomesha 'maafa ya kibinadamu' yanayowakabili Wapalestina wa ukanda huo.
-
Wazayuni wakiri kushindwa katika vita vya Gaza
Dec 28, 2023 00:51kuchukua muda mrefu vita vya Gaza kumewafanya, baadhi ya Wazayuni kukiri kushindwa utawala ghasibu wa Israel katika vita vyake vya jinai huko Gaza.
-
Israel yashambulia makao makuu ya Hilali Nyekundu Gaza
Dec 26, 2023 23:23Vikosi vya jeshi katili la utawala haramu wa Israel vimeshambulia kwa mabomu makao makuu ya Jumuiya ya Hilali Nyekundu ya Palestina katika Ukanda wa Gaza.
-
Waislamu US wamlaani Biden kwa kuunga mkono maangamizi ya kizazi Gaza
Dec 25, 2023 08:18Baraza la Mahusiano ya Kiislamu ya Marekani (CAIR) limeijia juu serikali ya Rais Joe Biden wa nchi hiyo kwa kile lilichokitaja kuwa ni 'mchango amilifu' wa Washington kwa mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala haramu wa Israel dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.
-
Balozi wa Iran: Ulaya ichukue hatua za maana kukomesha mauaji ya kimbari Gaza
Dec 25, 2023 07:12Balozi wa Iran nchini Iraq amesema nchi za Ulaya zinapasa kuchukua hatua za maana kwa ajili ya kukomesha jinai na mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala haramu wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
-
Mbali na kuua watoto wachanga, Wazayuni wanafanya uporaji pia Ghaza
Dec 23, 2023 23:09Mkuu wa Ofisi ya Upashaji Habari ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema kuwa mbali na jinai zao nyingine nyingine kama za kuua watoto wachanga, wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wanafanya uporaji pia wa mali za Wapalestina wakati wanapoingia kwenye nyumba walizozivunja kwa mashambulizi ya kikatili na kinyama huko Ghaza.
-
Watumishi wa umma Uholanzi waandamana wakitaka kusitishwa vita Gaza
Dec 22, 2023 22:57Makumi ya wafanyakazi wa umma nchini Uholanzi jana Ijumaa waliwashangaza wengi kwa kuingia mabarabarani kushiriki maandamano ya kutaka kutekelezwa usitishaji vita wa kudumu katika Ukanda wa Gaza.
-
Human Rights Watch: Meta inazuia sauti zinazowatetea Wapalestina kwenye Instagram na Facebook
Dec 21, 2023 23:36Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limesema kuwa sera za kamupini ya Meta zimezidi kuziba na kunyamazisha sauti zinazoiunga mkono Palestina kwenye mitandao ya kijamii ya Instagram na Facebook kutokana na vita vya Israel dhidi ya Gaza.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran azungumza na waziri mwenzake wa Afrika Kusini, Ghaza maudhui kuu
Dec 20, 2023 23:58Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amefanya mazungumzo ya simu na waziri mwenzake wa mambo ya nje wa Afrika Kusini na kujadiliana naye masuala mbalimbali muhimu ya pande mbili, ya kieneo na ya kimataifa na hasa vita vya Ghaza huko Palestina.