-
Israel yashadidisha mauaji dhidi ya wakazi wa Gaza; mashinikizo ya kimataifa yaongezeka dhidi yake
Sep 18, 2025 03:53Idadi ya vifo vya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza inaendelea kuongezeka huku mashambulizi ya kijeshi na mauaji ya kimbari ya Israel yakiingia mwaka wa pili sasa, na hivyo kuzidisha ukosoaji kimataifa.
-
Wabunge wa UK: Vikosi vya kijeshi vitakavyoongozwa na UN vipelekwe Ghaza kuzuia mauaji ya kimbari
Sep 18, 2025 00:16Wabunge watano wa Uingereza wamemwandikia barua waziri wao wa mambo ya nje Yvette Cooper wakiitaka serikali ya London "ifuatilie kwa dharura uingiliaji kati wa kijeshi utakaoongozwa na Umoja wa Mataifa" ili kukomesha mauaji ya kimbari ya yanayofanywa na Israel huko Ghaza.
-
Israel yashambulia kwa mabomu mnara wa 50 wa makazi katika mji wa Gaza
Sep 08, 2025 04:03Utawala wa Israel umeshadidisha mashambulizi yake ya kinyama katika Ukanda wa Gaza kwa kushambulia na kubomoa jengo jingine la mnara wa 50 wa makazi ya Wapalestina katika mji wa Gaza huku ikitekeleza mashambulizi ya nchi kavu kwa lengo la kulikalia kwa mabavu eneo hilo.
-
Jeshi la kizayuni laporomosha jengo la ghorofa 12 linalowapa hifadhi mamia ya Wapalestina Ghaza
Sep 05, 2025 23:36Jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel siku ya Ijumaa liliripua na kuporomosha jengo la ghorofa 12 la makazi ya raia magharibi mwa Mji wa Ghaza linalowapa hifadhi mamia ya Wapalestina waliolazimika kuyahama makazi yao katika eneo hilo lenye msongamano wa watu na ambalo limekuwa kimbilio la makumi ya maelfu ya Wapalestina.
-
IRIB yalaani mauaji ya mwanahabari wa Al-Alam huko Gaza
Sep 03, 2025 02:57Kitengo cha Kimataifa cha Shirika la Utangazaji wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran IRIB kimelaani vikali mauaji ya Rasmi Jihad Salem, mpigapicha wa kanali yake ya Kiarabu ya Al-Alam, ambaye aliuawa shahidi katika shambulio la Israel huko Gaza jana Jumanne, Septemba 2 alipokuwa akirejea kutoka kazini.
-
Norway yalaani jinai za Israel Ukanda wa Gaza
Aug 25, 2025 23:17Norway imeutaja ukatili unaofanya utawala wa Israel katika Ukanda wa Gaza kuwa ni ukiukaji wa wazi wa sheria za kimataifa, na kutangaza kwamba nchi hiyo ya Ulaya inafikiria kupiga marufuku makampuni ya Norway kushiriki katika shughuli zinazounga mkono upanuzi wa vitongoji vya walowezi katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Israel yaendelea kumwaga damu za wanahabari Gaza, yaua wengine 4
Aug 25, 2025 07:06Kwa akali wanahabari wanne wa Kipalestina, akiwemo mpiga picha wa televisheni ya Al-Jazeera, ni miongoni mwa watu 15 waliouawa shahidi katika shambulio jipya la Israel dhidi ya hospitali moja iliyoko kusini mwa Ukanda wa Gaza.
-
Wanahabari wa Afrika waunda Muungano wa Kupinga Mauaji ya Kimbari ya Israel Gaza
Aug 24, 2025 23:29Waandishi wa habari kutoka bara zima la Afrika wamezindua muungano uliopewa jina la 'African Journalists Against Genocide (AJAG)' wenye lengo la kupinga kile wanachoeleza kuwa ni mauaji ya kimbari ya Israel na uhalifu wa kivita dhidi ya watu wa Gaza, wakiwemo wanahabari wenzao.
-
WHO: Zaidi ya watu 15,600 wakiwemo watoto 3,800 wanahitaji kuondolewa haraka Gaza kwa ajili ya matibabu
Aug 24, 2025 08:23Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) ameeleza kuwa watu zaidi ya 15,600 katika Ukanda wa Gaza, wakiwemo watoto 3,800, wanahitaji kuondolewa haraka katika eneo hilo lililokumbwa na vita ili kupata huduma maalumu ya matibabu.
-
Hamas yaonya: Israel haitafikia malengo yake Ukanda wa Gaza
Aug 21, 2025 03:01Utawala wa Israel umeanza kupeleka vikosi vya jeshi lake kwenye viunga vya Jiji la Gaza kwa ajili ya kuanza kutekeleza mpango wake wa kukalia kwa mabavu eneo hilo kubwa zaidi la Ukanda wa Gaza, lakini Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imeonya kuwa, Tel Aviv itashindwa kutimiza malengo yake.