-
Iran yaitaka Vatican ichukue hatua za haraka kukomesha mauaji ya kimbari Gaza
May 24, 2025 03:40Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, katika mkutano na maafisa wa Makao Makuu ya Kanisa Katoliki Duniani, Vatican huko mjini Rome, ametoa wito wa kuchukuliwa hatua za haraka za kimataifa kukomesha uhalifu unaoendelea kufanyika Gaza, na kuhakikisha misaada ya kibinadamu inafika katika eneo hilo lililozingirwa.
-
Hamas yapongeza mataifa 80 kwa kulaani jinai za Israel huko Gaza
May 23, 2025 08:26Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imekaribisha kwa mikono miwili taarifa ya pamoja iliyotolewa na nchi 80 duniani, zikisisitiza kwamba Gaza inakabiliwa na mzozo mbaya zaidi wa kibinadamu tangu kuanza kwa vita vya Israel Oktoba 7 mwaka 2023.
-
Iran, Misri zataka kukomeshwa mashambulizi ya Israel huko Gaza
May 13, 2025 23:16Wanadiplomasia wakuu wa Iran na Misri wamesisitiza kuwa kuna haja ya kukomeshwa mashambulizi ya utawla wa Israel dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.
-
Israel yaendeleza ukatili Gaza, yaua shahidi Wapalestina wengine 33
May 12, 2025 08:30Wapalestina wasiopungua 33 wameuawa shahidi katika muda wa saa 24 zilizopita huko Gaza, maafisa wa afya katika eneo hilo lililo chini ya mzingiro wameripoti.
-
Israel: Hatusitishi mashambulizi mpaka Wapalestina wafukuzwe Gaza; Syria igawanyishwe
Apr 30, 2025 06:49Waziri wa fedha mwenye misimamo ya kuchupa mipaka wa Israel, Bezalel Smotrich anasema utawala huo wa Kizayuni utasitisha tu uvamizi wake Gaza wakati "mamia ya maelfu" ya Wapalestina watalazimishwa kuyahama makazi yao; na Syria igawanyishwe vipande vipande.
-
Makumi ya wanawake, watoto wauawa na mabomu ya Wazayuni Gaza
Apr 16, 2025 11:21Mashambulizi makali ya anga ya utawala wa Kizayuni wa Israel yameua shahidi zaidi ya Wapalestina 20, wakiwemo wanawake na watoto wadogo katika Ukanda wa Gaza.
-
UN: Wapalestina 400,000 Gaza wamefurushwa makwao ndani ya wiki 3
Apr 12, 2025 08:10Takwimu mpya za Umoja wa Mataifa zinaonyesha kuwa, idadi kubwa ya Wapalestina wamelazimika kuyahama makazi yao katika Ukanda wa Gaza tangu utawala haramu wa Israel uanzishe mashambulizi mapya baada ya kuvunja makubaliano ya usitishaji vita zaidi ya wiki tatu zilizopita.
-
Ripota wa UN: Muda wa kuwanusuru Wapalestina unazidi kuyoyoma
Apr 10, 2025 22:36Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya Palestina ameonya kwamba "hakuna muda mwingi uliobaki" kuwaokoa watu wa Palestina wakati huu ambapo Israel inaendeleza mashambulizi yake mtawalia katika Ukanda wa Gaza, na ukandamizaji unaoendelea katika Ukingo wa Magharibi.
-
Wapalestina wengine 40 wauawa shahidi Gaza na mabomu ya Wazayuni
Apr 09, 2025 23:24Utawala wa Kizayuni wa Israel umeendelea kumwaga damu za Wapalestina; ambapo umewauwa Wapalestina karibu 40 wakiwemo watoto katika mashambulizi ya anga ya karibuni katika maeneo kadhaa katika Ukanda wa Gaza unaozingirwa.
-
Watoto laki 6 wa Kipalestina Gaza katika hatari ya kupata ulemavu
Apr 07, 2025 08:06Wizara ya Afya katika Ukanda wa Gaza imesema hatua ya Israel ya kuzuia kampeni ya chanjo ya ugonjwa wa kupooza wa polio inawaweka malaki ya watoto wa Kipalestina katika hatari ya kupata ulemavu wa kudumu.