-
Baraza la Usalama laitaka Sudan Kusini iache kukwamisha shughuli za kikosi cha UN
Aug 25, 2017 09:15Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeitaka serikali ya Sudan Kusini iache kukwamisha shughuli za kikosi cha askari wa kofia buluu wa Umoja wa Mataifa walioko katika nchi hiyo changa zaidi barani Afrika.
-
Wahanga wa mashambulizi ya Boko Haram waongezeka nchini Niger
Aug 24, 2017 23:51Ofisi ya Uratibu wa Misaada ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa imesema kuwa, tangu yalipoanza mashambulizi ya kwanza ya genge la kigaidi la Boko Haram nchini Niger mwezi Februari 2015, karibu watu 540 imma wameuawa au kujeruhiwa au kutekwa nyara na kundi hilo la wakufurishaji.
-
Koffi Annan: Haki za Waislamu wa Rohingya nchini Myanmar ziheshimiwe
Aug 24, 2017 09:13Katibu Mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa amelaani vikali mauaji ya Waislamu wa Rohingya nchini Myanmar na kusisitiza kuwa, utumiaji wa mabavu na nguvu kupita kiasi dhidi yao hakuwezi kusaidia kuupatia ufumbuzi mgogoro wa nchi hiyo.
-
UN yatiwa wasiwasi na hali za wanawake wa Kiiraqi katika miji inayokaliwa kwa mabavu na Daesh
Aug 22, 2017 23:17Ujumbe wa misaada ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa ulioko nchini Iraq na ofisi ya haki za binadamu ya umoja huo zimetoa ripoti na kutangaza kuwa wanawake na wasichana wa Kiiraqi wanaoishi kwenye miji inayokaliwa kwa mabavu na kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh wanakabiliwa na ukiukaji wa haki za binadamu.
-
Sudan Kusini yapiga marufuku ndege za walinda amani wa UN kutumia uwanja wa Juba
Aug 22, 2017 10:57Serikali ya Sudan Kusini imepiga marufuku ndege za vikosi vya kulinda amani vya Umoja wa Mataifa kuruka kutokea uwanja wa ndege wa mji mkuu wa nchi hiyo, Juba.
-
Watoaji wa huduma za kibinadamu Sudan Kusini waendelea kushambuliwa
Aug 19, 2017 23:54Mratibu wa masuala ya kibiadamu nchini Sudan Kusini amesema kuwa mashambulizi dhidi ya watoaji wa huduma za kibiandamu nchini humo yameongezeka.
-
Katibu Mkuu wa UN akerwa na vita vya maneno kati ya US na Korea Kaskazini
Aug 17, 2017 03:12Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameeleza wasiwasi wake kuhusu kushtadi vita vya maneno kati ya Marekani na Korea Kaskazini na kusema kuwa, kuna haja ya pande mbili hizo kukumbatia diplomasia.
-
UN yaikosoa Marekani kwa kuwazuilia wahajiri na wanaotafuta hifadhi
Aug 14, 2017 23:26Wataalamu wa masuala ya haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa wamekosoa kitendo cha Marekani kuendelea kuwazuilia wahamiaji na raia wa kigeni wanaotafuta hifadhi nchini humo.
-
Hatimaye UN yavunja kimya chake, yaitaka Saudia iheshimu haki za binadamu
Aug 11, 2017 02:38Umoja wa Mataifa umeutaka utawala wa Aal-Saud nchini Saudi Arabia kukomesha jinai na mashambulio dhidi ya Waislamu wa madhehebu ya Shia mashariki mwa nchi hiyo.
-
UN: Tunafuatilia kwa karibu uchaguzi wa Kenya
Aug 08, 2017 03:21Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema umoja huo unafuatilia kwa karibu zoezi la uchaguzi mkuu linalofanyika hii leo nchini Kenya.