-
UN yaitaka Saudia iache kuwakandamiza watetezi wa haki za binadamu
Jan 03, 2018 00:31Wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa wameitaka Saudi Arabia ikomeshe ukandamizaji wa watetezi wa haki za binadamu nchini humo.
-
Kushtadi mauaji ya Saudi Arabia ikishirikiana na Marekani dhidi ya wananchi wa Yemen
Dec 30, 2017 04:39Mratibu wa masuala ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa nchini Yemen amekosoa vikali kuendelea kuuawa kiholela raia katika nchi hiyo, mauaji ambayo yamekuwa yakifanywa na muungano wa kijeshi unaoongozwa na Saudi Arabia.
-
Mwanamke Mualgeria ateuliwa kuwa mkuu wa kikosi cha MONUSCO DRC
Dec 28, 2017 12:56Bi Leila Zerrougui raia wa Algeria ameteuliwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuwa, mkuu wa kikosi cha kusimamia amani cha Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo MONUSCO.
-
Hali ya kifedha ya UN ni mbaya, maafisa 131 kufutwa kazi
Dec 27, 2017 23:12Msemaji wa Katibu Mkuu Umoja wa Mataifa amesema kuwa hali ya kifedha ya umoja huo ni mbaya hivyo kuna mpango wa kuwafuta kazi maafisa wake 131 kama njia ya kubana matumizi.
-
Velayati: Palestina ni kadhia nambari moja ya Ulimwengu wa Kiislamu
Dec 26, 2017 11:53Mshauri wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu katika Masuala ya Kimataifa ameeleza kuwa Palestina inaendelea kuwa suala la kwanza linalouhusu Ulimwengu wa Kiislamu.
-
Baraza Kuu la UN lalaani mauaji ya Mabudha dhidi ya Waislamu Myanmar
Dec 24, 2017 23:53Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limepasisha azimio kwa wingi wa kura likilaani jinai na mauaji yanayoendelea kufanywa na Mabudha wa Myanmar dhidi ya Waislamu wa jamii ya Rohingya nchini humo.
-
Gazeti la Israel la Haaretz: Kushindwa kwa Trump UN ni 'zawadi kwa Iran'
Dec 24, 2017 13:11Gazeti la Kizayuni la Haaretz limeandika kuwa kushindwa Rais Donald Trump wa Marekani kupata uungaji mkono katika Umoja wa Mataifa kuhusiana na uamuzi wake wa kuitambua Quds kuwa mji mkuu wa Israel ni sawa na 'kuipatia zawadi' Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Zarif: Trump anadunisha demokrasia kwa kutishia wapinzani wake
Dec 21, 2017 00:12Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran amekosoa vikali msimamo wa Marekani wa kupinga maamuzi ya Umoja wa Mataifa kuhusu Quds tukufu na kusema kuwa: Washington imebakia katika kiwango cha "ama uwe pamoja na sisi au dhidi yetu."
-
UN: Hujuma za anga za Saudia zimeua 136 Yemen ndani ya siku 11
Dec 19, 2017 23:05Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa (OHCHR) imesema mashambulizi ya anga yanayofanywa na ndege za kivita za Saudi Arabia dhidi ya Yemen yamesababisha vifo vya raia wasiopungua 136 katika muda wa siku 11.
-
Upinzani wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa ripoti iliyo dhidi ya Iran
Dec 18, 2017 23:18Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameipinga ripoti iliyo dhidi ya Iran iliyosambazwa na vyombo vya habari vya Marekani vinavyodai kuwa eti Iran imejaribu kununua kinyume cha sheria vipande vya makombora vinavyoweza kutumika kijeshi au katika masuala ya nyuklia kutoka kwa Ujerumani.