Sep 06, 2016 06:44
Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu jana Jumatatu alituma ujumbe maalumu kwa mnasaba wa ibada adhimu ya Hija na kueleza kwamba msimu wa Hija kwa Waislamu ni msimu wa kujivunia na wa adhama mbele ya macho ya viumbe; na ni msimu wa kunawirisha nyoyo na kudhihirisha khushuu na unyenyekevu mbele ya Muumba.