-
Larijani: Israel inafanya njama za kuzusha vurugu za kisiasa katika Mashariki ya Kati
Dec 18, 2017 10:44Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa, utawala dhalimu wa Israel unafanya njama za kuleta vurugu za kisiasa katika Mashariki ya Kati na kuongeza kuwa, endapo nchi za Kiislamu zitadumisha umoja na mshikamano zitazuia kufikiwa malengo hayo ya Wazayuni.
-
Dakta Velayati: Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haijaipatia kombora Yemen
Dec 18, 2017 01:12Mshauri wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu katika masuala ya kimataifa amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu haijaipatia kombora lolote Yemen.
-
Mtego wa Israel kwa Saudia, kuwatenga Aal Saud na ulimwengu wa Kiislamu
Dec 15, 2017 02:39Gazeti la Kizayuni la Haaretz limetangaza kuwa, Yisrael Katz, waziri wa masuala ya kijasusi wa utawala wa Kizayuni wa Israel amemwita mjini Tel Aviv, Muhammad bin Salman, mrithi wa kiti cha ufalme wa Saudi Arabia.
-
Wapalestina wapatao 1,800 wamejeruhiwa tangu Trump atoe tangazo kuhusu Quds, 6 wameshauawa shahidi Gaza
Dec 12, 2017 13:11Shirika la Hilali Nyekundu la Palestina limetangaza kuwa tangu yalipoanza maandamano ya kupinga uamuzi wa Rais wa Marekani Donald Trump wa kuitangaza Baitul Muqaddas kuwa mji mkuu wa utawala wa Kizayuni, hadi sasa Wapalestina 1,795 wamejeruhiwa katika Ukanda wa Gaza na Ufukwe wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Khalid Mash'al: Uamuzi wa Trump kuhusu Quds ni mwanzo wa kuangamia Israel
Dec 10, 2017 11:07Khalid Mash'al, Mkuu wa zamani wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema kuwa, uamuzi wa Rais Donald Trump wa Marekani wa kutoa amri ya kuhamishiwa ubalozi wa nchi yake huko Beitul-Muqaddas ni mwanzo wa kuangamia utawala ghasibu wa Israel.
-
Ayatullah Khamenei: Marekani, Israel na vibaraka wao Mashariki ya Kati ni mafirauni wa zama hizi
Dec 06, 2017 12:07Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, Marekani, utawala haramu wa Israel, wenye fikra mgando na wategemezi wa madola makubwa ni mafirauni wa zama hizi na kuongeza kuwa, baadhi ya wanasiasa wa Kimarekani wamekiri bayana kwamba, kuna ulazima wa kutokea vita na machafuko magharibi mwa Asia (Mashariki ya Kati) ili utawala ghasibu wa Israel uwe katika amani na wakati huo huo kuufanya ulimwengu uliotapakaa damu wa Kiislamu usipate maendeleo.
-
Nchi za Ulaya: Hatua ya Marekani dhidi ya Quds inatia wasiwasi
Dec 06, 2017 11:31Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Italia, Uingereza, Sweden na Ujerumani wamesema kuwa wana wasiwasi mkubwa na uamuzi wa upande mmoja wa Rais Donald Trump wa Marekani wa kuutambua rasmi mji wa Quds kama mji mkuu wa utawala wa Kizayuni.
-
Larijani: Iran na Russia kuendeleza ushirikiano wa kupambana na ugaidi
Dec 04, 2017 23:17Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, mazunguumzo ya Tehran na Moscow kuhusu kupambana na ugaidi na ushirikiano wa pamoja katika uwanja huo utaendelea.
-
Mwandishi wa gazeti la Haaretz: Israel ni moja ya tawala za kinyama zaidi duniani
Dec 02, 2017 11:24Mwandishi mmoja wa habari wa gazeti la Haaretz ameukosoa vikali utawala wa Kizayuni wa Israel kwa kusema kuwa: utawala wa Kizayuni ni moja ya tawala dhalimu na za kinyama zaidi duniani.
-
HAMAS: Makombora yetu yataendelea kuwatwanga Wazayuni
Nov 30, 2017 00:13Brigedi za Shahid Izzuddin Qassam, tawi la kijeshi la Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS zimesisitiza kuwa, silaha za muqawama zitaendelea kuelekezwa upande wa utawala wa Kizayuni wa Israel.