-
Ulimwengu waunga mkono ripoti ya UN kuhusu mauaji ya kimbari ya Israel Ukanda wa Gaza
Mar 27, 2024 08:36Tathmini iliyofanywa na Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa katika Masuala ya Palestina ambayo imezitaja jinai za utawala wa Kizayuni huko Ukanda wa Gaza kuwa ni mauaji ya kimbari imeungwa mkono pakubwa na nchi mbalimbali katika umoja huo.
-
Kiongozi Muadhamu: Muqawama usio na kifani wa vikosi vya Muqawama na watu wa Ghaza umeutukuza Uislamu
Mar 26, 2024 23:28Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema, Muqawama usio na kifani wa vikosi vya Muqawama na watu wa Ghaza umeutukuza Uislamu.
-
Kuendelea kushambuliwa na kuzingirwa hospitali za Gaza na utawala wa Kizayuni
Mar 26, 2024 22:36Licha ya wasiwasi mkubwa na maonyo ya mara kwa mara ya viongozi wa nchi mbalimbali na taasisi za kimataifa, utawala wa Kizayuni bado unaendelea kushambulia na kuzizingira hospitali za Gaza.
-
Ismail Haniya wa Hamas afika Tehran, akutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran
Mar 26, 2024 08:12Ismail Haniyah, mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas), leo amewasili Tehran na kukutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Hossein Amir Abdollahian ambapo wamejadili matukio ya hivi karibuni katika eneo la Ukanda wa Gaza.
-
Baraza la Usalama la UN lapasisha azimio la kusimamisha vita Gaza haraka iwezekanavyo
Mar 26, 2024 04:27Azimio la kusimamisha vita huko Ukanda wa Gaza hatimaye limepasishwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa baada ya miezi kadhaa ya mashambulizi ya jeshi la utawala wa Kizayuni katika eneo hilo.
-
Guterres akiri kashfa ya kimaadili ya utawala wa Kizayuni katika kuzuia misaada ya kibinadamu kuingia Gaza.
Mar 25, 2024 22:30Antonio Guterres, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, ametembelea kivuko cha Rafah (kati ya Ukanda wa Gaza na Misri), katika mwezi wa sita wa mauaji ya halaiki ya utawala wa Kizayuni huko Gaza, na kukitaja kitendo cha utawala huo wa Kizayuni cha kuzuia misaada ya kibinadamu kuingia Gaza kuwa ni "kashfa ya kimaadili".
-
Mkutano wa Umoja wa Mabunge unaendelea Geneva kwa kuhudhuriwa na Iran
Mar 25, 2024 08:31Mkutano wa Umoja wa Mabunge Duniani, kama chombo kikubwa zaidi cha utungaji sheria chenye nchi wanachama zaidi ya 180, ukiwemo ujumbe kutoka Iran unafanyika mjini Geneva Uswisi kwa kauli mbiu ya "Diplomasia ya Bunge, Ujenzi wa Daraja la Amani na Maelewano".
-
Kula mweleka njama za Marekani za kuunga mkono mauaji ya kimbari ya Israel kwenye UN
Mar 23, 2024 08:11Azimio lililopendekezwa na Marekani la kuunga mkono mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel huko Ghaza limegonga ukuta baada ya kupigiwa kura ya veto na Russia na China ndani ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
-
Wito wa maseneta 19 wa Marekani wa kuundwa taifa huru la Palestina
Mar 22, 2024 22:59Maseneta 19 wa chama cha Democratic wametoa wito wa kuundwa taifa huru la Palestina katika barua yao iliyotumwa kwa Rais wa Marekani, Joe Biden.
-
Iran yalaani shambulio katika hospitali ya Al Shifa Ukanda wa Gaza
Mar 19, 2024 08:21Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani kitendo cha ukatili na kinyama cha utawala wa Kizayuni cha kuishambulia hospitali ya al Shifa huko Ukanda wa Gaza.