-
29 wafa maji, 11 waokolewa katika ajali ya boti pwani ya Tunisia
Mar 27, 2023 11:35Gadi ya Kitaifa ya Ulinzi wa Pwani ya Tunisia imetangaza habari ya kuaga dunia wahamiaji 29 kati ya 34 wa Kiafrika waliotoweka Ijumaa iliyopita baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kuelekea Ulaya kuzama baharini karibu na pwani ya Tunisia.
-
Mamia ya wahajiri wa Kiafrika warejea nyumbani wakitokea Tunisia
Mar 05, 2023 10:39Mamia ya wahajiri wa Kiafrika wamerejea katika nchi zao wakitokea Tunisia, siku chache baada ya Rais Kais Saied wa nchi hiyo kutoa matamshi yaliyoonekana kuwa dhidi ya wahamiaji nchini humo.
-
Maiti 27 za wahajiri zapatikana jangwani nchini Chad
Dec 14, 2022 11:11Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) limetangaza habari ya kugunduliwa maiti za wahamiaji 27 zikiwemo za watoto wanne katika jangwa moja nchini Chad.
-
Maelfu ya wahajiri wamepigwa na kudhalilishwa katika mipaka ya EU
Dec 10, 2022 02:22Ripoti mpya iliyotolewa na shirika moja la kutetea haki za binadamu imefichua kuwa, maelfu ya wahajiri walipewa kichapo cha mbwa, baadhi wakadhalilishwa na wengine wakazuiliwa kinyume cha sheria kabla ya kurejeshwa waliokotoka na askari wa mipaka ya nchi za Umoja wa Ulaya.
-
Morocco yazuia wahajiri 56,000 kwenda Ulaya kupitia Mediterania
Nov 14, 2022 11:07Mamlaka za Morocco zimetangaza kuwa zimezima majaribio ya makumi ya maelfu ya wahamiaji haramu waliojaribu kuvuka bahari ya Mediterania kuelekea Ulaya.
-
Maiti 8 za wahajiri zapatikana pwani ya kusini ya Tunisia
Oct 11, 2022 11:51Wavuvi wa Tunisia wameopoa miili ya wahajiri wanane waliokufa maji katika pwani ya mji wa Zarzis, kusini mwa nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.
-
Maiti 20 za wahajiri zapatikana katika mpaka wa Libya na Sudan
Aug 13, 2022 11:24Maiti 20 za wahajiri haramu zimepatikana katika jangwa lililoko baina ya Libya na Sudan.
-
Makumi ya wahajiri wahofiwa kufa maji wakielekea Italia
Aug 10, 2022 11:22Makumi ya wahajiri wanahofia kuaga dunia baada ya boti yao kuzama wakijaribu kuelekea Italia.
-
Maiti 20 za wahajiri zapatikana jangwani nchini Libya
Jun 30, 2022 07:52Maiti 20 za wahajiri walioripotiwa kutoweka katika jangwa nchini Libya karibu na mpaka wa Chad, zimepatikana kusini mashariki mwa nchi.
-
Morocco: Wahajiri 18 wameaga dunia wakijaribu kuingia eneo la Melilla la Uhispania
Jun 25, 2022 11:47Serikali ya Morocco imesema wahajiri 18 wamepoteza maisha, huku makumi ya wengine pamoja na askari polisi wakijeruhiwa katika mkanyagano wa kujaribu kuingia katika maeneo ya Melilla na Ceuta yanayodhibitiwa na Uhispania.