-
Mkutano wa 34 wa kimataifa wa Umoja wa Kiislamu kufanyika Tehran
Oct 27, 2020 12:32Mkutano wa 34 wa Kimataifa wa Umoja wa Kiislamu unatazamiwa kuanza Alhamisi katika mji mkuu wa Iran, Tehran ambapo mada kuu itakuwa 'Ushirikiano wa Kiislamu Wakati wa Maafa na Majanga'.
-
HAMAS: Chokochoko za Ufaransa zimeumiza hisia za Waislamu duniani
Oct 26, 2020 11:44Afisa mmoja wa ngazi za juu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) amesema hatua za kichochezi na kichokozi za maafisa wa serikali ya Ufaransa za kuunga mkono kuvunjiwa heshima Mtume Muhammad SAW na matukufu ya Kiislamu zimeumiza hisia na nyoyo za Waislamu kote duniani.
-
Ufaransa yamshambulia na kumtia mbaroni kiongozi wa taasisi ya Kiislamu
Oct 16, 2020 07:47Polisi ya Ufaransa imevamia nyumba ya kiongozi wa asasi moja isiyo ya kiserikali ya Waislamu wa nchi hiyo na kumtia mbaroni, katika kile kinachoonekana ni muendelezo wa hujuma dhidi ya Uislamu na Waislamu wa nchi hiyo ya Ulaya.
-
Jumuiya ya Kimataifa ya maulama wa Kiislamu yapinga matamshi ya Rais wa Ufaransa kuhusu Uislamu
Oct 04, 2020 02:47Mkuu wa Jumuiya ya Muungano wa Kimataifa wa Wanazuoni wa Kiislamu amejibu matamshi ya kihasama ya Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa kuhusu Uislamu na kusema kuwa Uislamu hauko wala hautakuwa katika mgogoro.
-
Jitihada za Macron za kuhalalisha muswada dhidi ya Uislamu nchini Ufaransa
Oct 04, 2020 02:43Hujuma na vitendo vya chuki dhidi ya Uislamu barani Ulaya viliongezeka sana baada ya matukio ya Septemba 11 mwaka 2001 nchini Marekani; na mashambulizi ya kundi la kigaidi na lenye misimamo mikali la Daesh katika baadhi ya nchi za Ulaya kama Ufaransa na Uingereza yamezidisha chuki na uhasama dhidi ya Waislamu. Hivi sasa serikali ya Ufaransa ina mpango wa kupasisha sheria ya kuimarisha hujuma na vita dhidi ya Uislamu.
-
China yakadhibisha madai ya kuvunja maelfu ya misikiti ya Waislamu wa Uighurs
Sep 27, 2020 04:40Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya China imekadhibisha madai yaliyotolewa na Taasisi ya Sera za Kistratejia ya Australia (The Australian Strategic Policy Institute) ASPI ikisema kuwa makumi ya misikiti imebomolewa katika eneo la Xinjiang lililoko kaskazini magharibi mwa nchi hiyo.
-
Wabunge wenye chuki wa Ufaransa wahamakishwa na hijabu bungeni
Sep 21, 2020 02:26Katika kile kinachoonekana ni muendelezo wa chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu barani Ulaya, mbunge mmoja wa chama tawala cha Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa ameongoza wabunge wenzake kutoka kwenye ukumbi wa bunge, eti kulalamikia uwepo wa mwanafunzi aliyevalia hijabu ndani ya taasisi hiyo ya taifa ya kutunga sheria.
-
Waislamu Canada wataka uchunguzi wa mauaji ya mwenzao nje ya msikiti Toronto
Sep 19, 2020 12:43Baraza la Kitaifa la Waislamu nchini Canada limetoa mwito wa kuchunguzwa mauaji ya Muislamu nje ya msikiti mmoja mjini Toronto, na kusisitiza kuwa mauaji hayo yamecochewa na chuki za kidini.
-
Amnesty International: Polisi ya India ilishirikiana na magenge ya Wahindu kuwashambulia Waislamu
Aug 31, 2020 02:33Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limesema jeshi la polisi la India lilifanya ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu kwa kushirikiana na magenge ya Wahindu wenye misimamo ya kufurutu mipaka kuwashambulia Waislamu katika mji mkuu New Delhi mapema mwaka huu.
-
Katibu Mkuu wa UN aikosoa serikali ya India kwa ubaguzi inaowafanyia Waislamu wa nchi hiyo
Aug 23, 2020 03:19Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameikosoa serikali ya India kwa ubaguzi inaowafanyia Waislamu wa nchi hiyo.