-
EuroMed Rights yakosoa chuki na uhasama Wa viongozi wa Ufaransa dhidi ya Waislamu
Oct 28, 2020 23:25Kituo cha Haki za Binadamu Ulaya na Mediterania (EuroMed Rights) kimeItaja hatua ya viongozi wa Ufaransa ya kueneza chuki na uhasama dhidi ya Waislamu kuwa ni hatari kubwa.
-
Radiamali ya kindumakuwili ya Ufaransa kufuatia malalamiko ya Waislamu duniani
Oct 28, 2020 04:11Waislamu duniani kote wamekasirishwa na kushadidi vitendo vya chuki dhidi ya Uislamu nchini Ufaransa hasa cha kuchapishwa tena katuni zinazomvunjia heshima Mtume Muhammad SAW. Hasira za Waislamu zimeongezeka maradufu baada ya Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa kutetea vitendo hivyo vya chuki dhidi ya Uislamu kwa kisingizo cha uhuru wa maoni.
-
Mkutano wa 34 wa kimataifa wa Umoja wa Kiislamu kufanyika Tehran
Oct 27, 2020 09:02Mkutano wa 34 wa Kimataifa wa Umoja wa Kiislamu unatazamiwa kuanza Alhamisi katika mji mkuu wa Iran, Tehran ambapo mada kuu itakuwa 'Ushirikiano wa Kiislamu Wakati wa Maafa na Majanga'.
-
HAMAS: Chokochoko za Ufaransa zimeumiza hisia za Waislamu duniani
Oct 26, 2020 08:14Afisa mmoja wa ngazi za juu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) amesema hatua za kichochezi na kichokozi za maafisa wa serikali ya Ufaransa za kuunga mkono kuvunjiwa heshima Mtume Muhammad SAW na matukufu ya Kiislamu zimeumiza hisia na nyoyo za Waislamu kote duniani.
-
Ufaransa yamshambulia na kumtia mbaroni kiongozi wa taasisi ya Kiislamu
Oct 16, 2020 04:17Polisi ya Ufaransa imevamia nyumba ya kiongozi wa asasi moja isiyo ya kiserikali ya Waislamu wa nchi hiyo na kumtia mbaroni, katika kile kinachoonekana ni muendelezo wa hujuma dhidi ya Uislamu na Waislamu wa nchi hiyo ya Ulaya.
-
Jumuiya ya Kimataifa ya maulama wa Kiislamu yapinga matamshi ya Rais wa Ufaransa kuhusu Uislamu
Oct 03, 2020 23:17Mkuu wa Jumuiya ya Muungano wa Kimataifa wa Wanazuoni wa Kiislamu amejibu matamshi ya kihasama ya Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa kuhusu Uislamu na kusema kuwa Uislamu hauko wala hautakuwa katika mgogoro.
-
Jitihada za Macron za kuhalalisha muswada dhidi ya Uislamu nchini Ufaransa
Oct 03, 2020 23:13Hujuma na vitendo vya chuki dhidi ya Uislamu barani Ulaya viliongezeka sana baada ya matukio ya Septemba 11 mwaka 2001 nchini Marekani; na mashambulizi ya kundi la kigaidi na lenye misimamo mikali la Daesh katika baadhi ya nchi za Ulaya kama Ufaransa na Uingereza yamezidisha chuki na uhasama dhidi ya Waislamu. Hivi sasa serikali ya Ufaransa ina mpango wa kupasisha sheria ya kuimarisha hujuma na vita dhidi ya Uislamu.
-
China yakadhibisha madai ya kuvunja maelfu ya misikiti ya Waislamu wa Uighurs
Sep 27, 2020 01:10Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya China imekadhibisha madai yaliyotolewa na Taasisi ya Sera za Kistratejia ya Australia (The Australian Strategic Policy Institute) ASPI ikisema kuwa makumi ya misikiti imebomolewa katika eneo la Xinjiang lililoko kaskazini magharibi mwa nchi hiyo.
-
Wabunge wenye chuki wa Ufaransa wahamakishwa na hijabu bungeni
Sep 20, 2020 22:56Katika kile kinachoonekana ni muendelezo wa chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu barani Ulaya, mbunge mmoja wa chama tawala cha Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa ameongoza wabunge wenzake kutoka kwenye ukumbi wa bunge, eti kulalamikia uwepo wa mwanafunzi aliyevalia hijabu ndani ya taasisi hiyo ya taifa ya kutunga sheria.
-
Waislamu Canada wataka uchunguzi wa mauaji ya mwenzao nje ya msikiti Toronto
Sep 19, 2020 08:13Baraza la Kitaifa la Waislamu nchini Canada limetoa mwito wa kuchunguzwa mauaji ya Muislamu nje ya msikiti mmoja mjini Toronto, na kusisitiza kuwa mauaji hayo yamecochewa na chuki za kidini.