Feb 19, 2023 02:25
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ametupilia mbali maelezo yaliyomo kwenye taarifa ya kikao cha tatu cha jopo kazi la pamoja la Marekani na Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi (GCC) kuhusu Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, na kueleza kwamba kutolewa taarifa kama hiyo kunaendana na mkakati wa muda mrefu wa utawala wa Marekani wa kuzusha mfarakano kati ya nchi za eneo hili.