-
Iran: Kutumiwa kisiasa IAEA kutatufanya tutoe jibu tofauti
Sep 06, 2021 02:51Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameionya vikali Bodi ya Magavana ya Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) dhidi ya kufanya mahesabu ghalati katika mkutano wake ujao na kusisitiza kuwa, kutumiwa kama jukwaa la kisiasa taasisi hiyo kutailazimisha Tehran itoe jibu tofauti.
-
Rais wa Iran amemteua Eslami kuwa Mkuu mpya wa AEOI
Aug 29, 2021 22:00Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amemteua Mohammad Eslami kuwa Mkuu mpya wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (AEOI).
-
Algeria: Ufaransa inakataa kutoa ramani ya maeneo yaliyotumiwa kwa majaribio ya nyuklia
Jul 05, 2021 05:49Waziri wa Mujahideen (maveterani wa vita vya ukombozi) nchini Algeria, Tayeb Zitouni amesema kuwa Ufaransa inakataa kuikabidhi nchi hiyo ramani ya maeneno yaliyotumiwa kwa ajili ya majaribio ya milipuko ya nyuklia yaliyofanywa na serikali ya Paris katika majangwa ya Algeria kwenye miaka ya sitini ya karne iliyopita.
-
Iran yaonya dhidi ya misimamo hasi ya wakala wa IAEA
Jun 07, 2021 23:09Balozi na mwakilishi wa kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika asasi za kimataifa zenye makao yao mjini Vienna Austria ametahadharisha kuhusu misimamo hasi na ya uhasama ya Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) dhidi ya Tehran.
-
Iran yajibu matamshi ya kuingilia masuala yake ya ndani yaliyotolewa na Arab League na GCC
Apr 16, 2021 22:14Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ameiasa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu na Baraza la Ushirikiano wa Ghuba ya Uajemi (P) GCC badala ya kuungana na utawala wa Kizayuni wa Israel katika kutoa tuhuma kila mara dhidi ya Iran zielekeze macho yao kwa shughuli za kijeshi za nyuklia na zilizo kinyume na sheria zinazofanywa na utawala huo.
-
Iran yaanza operesheni ya kuzalisha urani iliyorutubishwa kwa asilimia 60
Apr 13, 2021 22:47Msemaji wa Shirika la Atomiki la Iran amestangaza kuwa Jamhuri ya Kiislamu imeutumia barua Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) ikiujulisha kuwa inaanza operesheni ya kuzalisha madini ya urani yaliyorutubishwa kwa asilimia 60.
-
Zarif: Kukishambulia kituo cha nyuklia cha Iran ni jinai ya kivita
Apr 13, 2021 02:26Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kitendo cha Jumapili alfajiri cha kushambuliwa kwa makusudi mfumo wa usambazaji umeme wa kituo cha urutubishaji urani cha kituo cha nyuklia cha Natanz hapa nchini ni jinai ya kivita.
-
Rouhani: JCPOA imeipa uhalali sekta ya nyuklia ya Iran
Apr 10, 2021 08:03Rais Hassan Rouhani wa Iran amesema kupasishwa kwa makubaliano ya nyuklia ya Iran maarufu kama JCPOA kuliipa uhalali kamili wa kisheria sekta ya nyuklia ya taifa hili.
-
Iran yazindua mafanikio 133 katika Siku ya Kitaifa ya Teknolojia ya Nyuklia
Apr 10, 2021 08:01Mafanikio 133 ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika uga wa teknolojia ya nyuklia yamezinduliwa leo katika sherehe maalumu zilizofanyika kwa njia ya video kwa mnasaba wa Siku ya Kitaifa ya Teknolojia ya Nyuklia.
-
Iran: Kuchelewa kutuondolea vikwazo ni kwa maslahi ya mradi wetu wa nyuklia
Apr 10, 2021 03:33Msemaji wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran amesema kuchelewesha kuliondolea taifa hili vikwazo ni kwa maslahi ya mradi wa nyuklia wenye malengo ya amani wa Jamhuri ya Kiislamu.