-
Khatibzadeh: Huu si wakati mwafaka wa kuitishwa kikao cha JCPOA
Feb 28, 2021 23:44Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje wa Iran amesema kuwa, kwa kutilia maanani misimamo na hatua za karibuni za nchi tatu za Ulaya na Marekani, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaona kuwa huu si wakati mwafaka wa kufanyika kikao kisicho rasmi kilichopendekezwa na Mkuu wa Siasa za Nje za Umoja wa Ulaya baina ya nchi hizo na Tehran kuhusu kadhia ya mapatano ya nyuklia ya JCPOA.
-
AEIO yasema Iran itazindua miradi 50 ya nyuklia karibuni
Feb 09, 2021 23:00Mkuu wa Taasisi ya Atomiki ya Iran (AEOI) amesema Jamhuri ya Kiislamu itazindua miradi 50 ya mafanikio ya sekta ya nyuklia ya taifa hili karibuni hivi.
-
Iran kuzalisha kilo 9 za urani iliyorutubishwa kwa 20% kwa mwezi
Jan 06, 2021 01:12Mkuu wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran (AEOI) Ali Akbar Salehi amesema kuanzia sasa Jamhuri ya Kiislamu itakuwa inazalisha kilo tisa za urani iliyorutubishwa kwa kiwango cha asilimia 20 kila mwezi.
-
Mkuu wa IAEA: Iran inataka kuona dunia yenye usalama na uthabiti
Dec 17, 2020 04:08Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) amesema hamu kubwa ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni kuona usalama na uthabiti vinatawala duniani kote, na kwamba Tehran iko tayari kufanya mazungumzo amilifu na mataifa ambayo yapo tayari kufuata njia ya mazungumzo.
-
Iran yataka Baraza la Usalama la UN lichunguze mauaji ya Fakhrizadeh
Nov 29, 2020 08:50Naibu Waziri wa Sheria wa Iran ametoa wito kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuchunguza mauaji ya mwanasayansi wa nyuklia wa Iran shahidi Mohsen Fakhrizadeh.
-
Russia kuanzisha kambi ya jeshi nchini Sudan, itakuwa na meli za nyuklia
Nov 12, 2020 06:44Serikali ya Russia imechapisha hati ya makubaliano yake ya Sudan yanayoiruhusu Moscow kujenga kambi ya kijeshi na misaada ya kilojestiki ya jeshi la majini la nchi hiyo nchini Sudan ambacho kitakuwa na askari na maafisa 300 wa kijeshi.
-
UN yatangaza kuanza kutekelezwa mkataba wa kuzuia silaha za nyuklia
Oct 25, 2020 04:33Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa nchi nyingine 50 zimepasisha utekelezaji wa mkataba unaopiga marufuku silaha za nyuklia.
-
Kukiri mshauri wa usalama wa taifa wa Marekani malengo halisi ya Washington dhidi ya Iran
Oct 18, 2020 23:00Tarehe 8 Mei 2018 Marekani chini ya utawala wa Donald Trump, ilijitoa kwenye mapatano ya kimataifa ya nyuklia ya JCPOA na kuiwekea Iran vikwazo vikubwa zaidi ambavyo havijawahi kutokea. Ijapokuwa awali serikali ya Trump ilidai kuwa inataka mapatano ya nyuklia ya JCPOA yaangaliwe upya ndio maana imejitoa kwenye makubaliano hayo, lakini hivi sasa inatangaza waziwazi lengo lake hasa la kujitoa kwenye mapatano hayo.
-
Onyo la Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu hatari ya kutokea maafa ya nyuklia duniani
Oct 05, 2020 03:35Kuongezeka maghala ya silaha za nyuklia na mashindano ya kuboresha silaha hizo ni jambo linalohatarisha usalama wa dunia, suala ambalo limeupelekea Umoja wa Mataifa kutangaza wazi wasiwasi wake kuhusiana na hatari hiyo.
-
Gharib Abadi: Shughuli za nyuklia za Iran zina uwazi zaidi kuliko za nchi nyingine zote wanachama wa IAEA
Sep 17, 2020 08:46Balozi na mwakilishi wa kudumu wa Iran katika mashirika ya kimataifa yenye makao yao mjini Vienna amesema asilimia 22 ya ukaguzi wote uliofanywa duniani na Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA imefanyiwa Iran na akaeleza kwamba Tehran ndiyo inayoendesha kwa uwazi zaidi shughuli zake za nyuklia zenye malengo ya amani kuliko nchi zote wanachama wa wakala huo.