-
Dakta Abu Safiya anakabiliwa na hali mbaya katika gereza la Israel
Jul 05, 2026 11:00Shirika la Kimataifa la Haki za binadamu limearifu kuwa Dakta Hussam Abu Safiya, Mkurugenzi wa Hospitali ya Kamal Adwan huko Gaza ambaye amekuwa mikononi mwa Israel tangu mwaka 2024 anakabiliwa na tishio kubwa kwa maisha yake.
-
Korea Kaskazini yalifanyia majaribio kombora la kimkakati la kruzi na silaha nyingine
Jul 05, 2026 10:57Korea Kaskazini imelifanyia jaribio kombora la kimkakati la kruzi na silaha nyingine kutoka katika meli yake mpya ya kivita ya Kang Kon yenye yenye uzito wa tani 5,000 na refu wa mita 140. Shirika Kuu la Habari la Korea Kaskazini KCNA leo limetangaza kuwa Kiongozi wa nchi hiyo Kim Jong Un alisimamia majaribio hayo siku ya Ijumaa.
-
Hamas: Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa' ilibadilisha milinganyo yote ya kisiasa na kijeshi
Jul 05, 2026 03:46Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano ya Kisiasa na Vyombo vya Habari cha Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) nchini Lebanon amesema kuwa 'Operesheni ya 'Kimbunga cha Al-Aqsa' ilibadilisha milinganyo yote ya awali ya kisiasa na kijeshi, huku akisisitiza kuwa istiqama na mapambano ya taifa la Palestina vinapaswa kuenziwa kwa siku 1,000 baada ya kuanza operesheni hiyo kubwa dhidi ya Israel.
-
Umoja wa Mataifa watahadharisha juu ya janga la haki za binaadamu al-Obeid
Jul 04, 2026 04:12Mkuu wa shirika la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa Volker Turk ametahadharisha juu ya janga jingine la haki za binaadamu katika mji wa al-Obeid, nchini Sudan na kuutolea wito ulimwengu kuchukua hatua haraka iwezekanavyo.
-
Iran yaonya mataifa ya Ghuba ya Uajemi baada ya kikao kilichosimamiwa na Marekani nchini Bahrain
Jul 03, 2026 09:00Iran imetoa onyo kwa nchi za kikanda kuwa zichukue tahadhari ya juu dhidi ya mipango ya usalama inayoongozwa na Marekani, ikisema kuwa nchi hizo zisizahau athari za uvamizi wa kijeshi wa hivi karibuni wa Marekani na Israel uliovuruga usalama katika ukanda mzima wa Asia Magharibi.
-
Wapalestina wasisitiza haki ya kujilinda huku Gaza ikitimiza siku 1,000 za mauaji ya kimbari
Jul 03, 2026 08:25Makundi ya kupigania ukombozi wa Palestina yamesisitiza kuhusu “haki ya Wapalestina kupinga uvamizi kwa namna yoyote ile” na kukataa “usimamizi wowote wa kigeni” katika mambo ya ndani ya Palestina, wakati Gaza ikifikisha siku ya 1,000 ya mauaji ya kimbari yanayotekelezwa na utawala katili Israel ambayo yamesababisha vifo vya zaidi ya Wapalestina wasipungua 73,000.
-
Israel yatuma zana za kijeshi Somalia kupitia Nairobi
Jul 03, 2026 03:29Vyanzo vya ngazi ya juu vya kimkakati katika kanda vimeeleza kuwa shehena ya zana za kijeshi iliyotoka katika maeneo yanayokaliwa kwa mabavu na Israel imesafirishwa hadi Somalia kwa jina la ofisi ya Umoja wa Mataifa (UN).
-
Wanajeshi katili wa Israel wamuuwa kipa Mpalestina huko Gaza
Jul 02, 2026 11:43Wanajeshi wa Israel wameuuwa shahidi kwa risasi kipa wa Kipalestina katika Ukanda wa Gaza, na hivyo kuifanya idadi ya wanamichezo waliouliwa shahidi na jeshi la Israel kufikia 1,009.
-
Namna Watoto Wachanga wa Kipalestina Walivyogeuzwa Kuwa Walengwa wa Jinai za Kivita
Jul 02, 2026 10:36Ripoti mpya ya Tume Huru ya Kimataifa ya Uchunguzi ya Umoja wa Mataifa kuhusu ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na utawala ghasibu wa Israel imefichua mwelekeo mpya wa vita kwa kuwasilisha ushahidi wa kulengwa kimfumo watoto wachanga huko Gaza.
-
Wabunge wa Israel warushiana makonde ndani ya ukumbi wa Bunge
Jul 01, 2026 03:35Vyombo vya habari vya utawala wa Kizayuni vimeripoti kutokea vurugu na mapigano ndani ya Bunge la utawala huo (Knesset), kufuatia kufutwa sheria iliyokuwa inahusu wafungwa wa Kipalestina.