-
Hatua ya Israel ya kubomoa makao makuu ya UNRWA yaendelea kulaaniwa kimataifa
Jan 29, 2026 03:46Mawaziri wa mambo ya nje wa nchi tisa za Ulaya, pamoja na Kanada na Japan, wamelaani vikali hatua ya utawala wa Kizayuni wa Israel ya kubomoa makao makuu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Palestina (UNRWA) katika mji wa Baitul Muqaddas Mashariki unaokaliwa kwa mabavu.
-
HAMAS: Hakuna suala la upokonyaji silaha madamu uvamizi na ukaliaji wa ardhi unaendelea
Jan 28, 2026 11:05Afisa mwandamizi wa ofisi ya kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS, amejibu vitisho vilivyotolewa na waziri mkuu wa utawala wa kizayuni wa Israel kuhusu upokonyaji silaha huko Ghaza na kusisitiza kwamba, silaha za Muqawama zinahusiana na mwendelezo wa uvamizi na kukaliwa ardhi za Palestina kwa mabavu, na kwamba huo ni uamuzi wa kitaifa ambao hautaachwa hadi uvamizi utakapokomeshwa.
-
Trump atishia kuikatia misaada Iraq endapo Nouri al-Maliki atakuwa Waziri Mkuu
Jan 28, 2026 10:28Rais wa Marekani Donald Trump amedai katika ujumbe unaoakisi uingiliaji wa wazi wa masuala ya ndani ya Iraq kwamba Nouri al-Maliki hapasi kuwa waziri mkuu, kwa sababu kama atachaguliwa kushika wadhifa huo, Marekani haitatoa tena misaada kwa nchi hiyo.
-
Yemen yatoa onyo la kuishambulia manowari ya Marekani ikikiuka mzingiro wa Bahari Nyekundu
Jan 28, 2026 10:20Harakati ya Ansarullah ya Yemen, leo imetoa indhari kwa kukumbusha shambulio lake la huko ililofanya kwa mafanikio dhidi ya meli ya mafuta ya Uingereza ya "Marlin Luanda" katika Ghuba ya Aden kufuatia ukiukaji wa mzingiro wa majini uliowekwa na harakati hiyo dhidi ya Israel,
-
Jinai mpya: Hamas yailaani Israel kwa kufukua mamia ya makaburi huko Gaza
Jan 28, 2026 07:38Harakati ya muqawama ya Palestina, Hamas, imelaani jinai mpya ya utawala mhalifu wa Israel, ikisema kuwa wanajeshi wa Israel wamefukua mamia ya makaburi katika eneo la mashariki la Ukanda wa Gaza unaozingirwa. Wanajeshi wa utawala wa Kizyauni wamefukua makaburi ya Wapalestina wakitafuta mwili wa mateka wa mwisho wa utawala huo.
-
Katibu Mkuu wa Hizbullah asema hawatakuwa watazamaji katika uchokozi wowote dhidi ya Iran
Jan 27, 2026 06:39Katibu Mkuu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesisitiza kwa kusema: "Imam Khamenei, Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran ni Faqihi wetu Mtawala na sisi hatutabaki kuwa watazamaji mbele ya uchokozi wowote utakaofanywa dhidi ya Iran".
-
Mwanamke Muisraeli ashtuka kujiona kwenye orodha ya 'waliofariki' kwenye machafuko ya Iran
Jan 27, 2026 06:38Kijana wa kike wa kiisraeli aitwaye Noya Zion ameshtuka baada ya kuona picha yake inaonyeshwa kwenye televisheni ya taifa ya Israel kama mmoja wa watu waliouawa katika maandamano nchini Iran, mkasa ambao umezidi kudhihirisha jinsi utawala huo wa kizayuni unavyosambaza habari feki na za uwongo kuhusu machafuko ya hivi karibuni nchini Iran na namna serikali ya Jamhuri ya Kiislamu ilivyokabiliana nayo.
-
Ulimwengu unasubiri siku ya ghadhabu duniani kuunga mkono wafungwa wa Kipalestina
Jan 27, 2026 02:33Kampeni za kimataifa na za haki za binadamu zimetoa wito kwa watu huru duniani kote kushiriki katika mkusanyiko mkubwa wa kimataifa tarehe 31 Januari kwa ajili ya kuwaunga mkono Wafungwa wa Kipalestina.
-
Kata'ib Hizbullah yatoa wito kwa wanamuqawama kujiandaa kwa 'vita' ili kuinga mkono Iran
Jan 26, 2026 06:36Harakati ya Kata’ib Hizbullah ya Iraq (Brigedi za Hizbullah) imetangaza kuwa iko tayari kushiriki katika vita vyovyote vitakavyotokea ili kuilinda Iran, ikitoa wito kwa wanamapambano duniani kote kujiandaa kwa ajili ya hilo.
-
Bangladesh yalaani India kumruhusu waziri mkuu mtoro Hasina kutoa hotuba ya hadhara
Jan 26, 2026 03:48Bangladesh imesema "imeshangazwa" na "kushtushwa" kuona India imemruhusu waziri mkuu wa zamani mtoro Sheikh Hasina kutoa hotuba ya hadhara mjini New Delhi.