Jan 10, 2017 08:20 UTC
  • Viongozi mbali mbali duniani waomboleza kifo cha Ayatullah Rafsanjani

Huku shughuli za kumzika Mkuu wa Halmashauri ya Kuainisha Maslahi ya Mfumo wa Kiislamu hapa nchini, Ayatullah Akbar Hashemi Rafsanjani zikiendelea, shakhsia na viongozi mbali mbali wameendelea kutoa salamu zao za rambirambi kufuatia kifo cha mwanachuoni huyo.

Miongoni mwa shakhsia waliotuma salamu zao za rambirambi kwa familia, jamaa, na marafiki wa marehemu Rafsanjani pamoja na serikali na taifa la Iran kwa ujumla ni Rais Alassane Ouattara wa Ivory Coast na mwenzake wa Cuba, Raúl Castro. 

Rais wa Kodivaa

Wengine wa hivi punde kutuma salamu zao za pole ni Rais Bashar al-Assad wa Syria, Karen Karapetyan, Waziri MKuu wa Armenia, Mfalme Abdullah II wa Jordan na Rais wa eneo la Kurdistan nchini Iraq Masoud Barzani.

Katika ujumbe wake uliotumwa kwa Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Rais Abdelaziz Bouteflika wa Algeria amesema, taifa na serikali ya Algeria inatoa mkono wa pole kwa taifa na serikali ya Iran kutokana na kifo cha Ayatullah Rafsanjani. Awali pia Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini alituma salamu zake za rambirambi na kusema: "Afrika Kusini inamshukuru Rais (Mstaafu) Rafsanjani kwa moyo wake wa kujitolea kuimarisha uhusiano wa kibiashara na kisiasa na nchi za Afrika ikiwemo Afrika Kusini hususan wakati alipokuwa Rais wa Iran"

Josh Earnest, Katibu wa Masuala ya Vyombo vya Habari ya Ikulu ya Marekani White House

Hali kadhalika Josh Earnest, Katibu wa Masuala ya Vyombo vya Habari ya Ikulu ya Marekani White House ametuma rambirambi zake akimtaja Rafsanjani kama shakhsia wa aina yake katika historia ya Iran.

Ayatullah Akbar Hashemi Rafsanjani alifariki dunia juzi usiku akiwa na umri wa miaka 82, baada ya kukumbwa na mshtuko wa moyo.

Tags