-
Rais Hassan Rouhani atangazwa kuwa mshindi wa uchaguzi wa jana
May 20, 2017 05:36Tume ya uchaguzi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, imemtangaza Rais Hassan Rouhani kuwa mshindi wa duru ya 12 ya uchaguzi wa rais iliyofanyika Ijumaa ya jana kwa kupata asilimia 57.
-
Rais Hassan Rouhani aendelea kuongoza katika matokeo ya pili ya uchaguzi wa jana
May 20, 2017 03:44Kwa mujibu wa matokeo ya awamu ya pili ya uchaguzi wa rais wa duru ya 12 nchini Iran, Rais Hassan Rouhani ameendelea kuongoza kwa kupata zaidi ya kura milioni 22.
-
Rais Rouhani anaongoza katika matokeo ya awali, akifuatiwa na Raeisi
May 19, 2017 23:30Zoezi la kuhesabu kura za uchaguzi uliofanyika jana hapa nchini Iran linaendelea na matokeo ya awali yanaonyesha kuwa, Rais wa sasa Hassan Rouhani anaongoza akifuatiwa na Sayyid Ibrahim Raeisi.
-
Muda wa upigaji kura katika uchaguzi wa rais wa Iran waongezwa
May 19, 2017 12:07Tume ya Uchaguzi nchini Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, imeongeza muda wa kupiga kura katika uchaguzi wa duru ya 12 ya urais.
-
Ayatullah Kermani apongeza ushiriki mkubwa wa wananchi wa Iran katika uchaguzi wa leo
May 19, 2017 11:54Khatibu wa Sala ya Ijumaa iliyoswaliwa leo mjini Tehran amepongeza ushiriki mkubwa wa wananchi katika upigaji kura wa uchaguzi wa rais leo na kusema kuwa, suala hilo ni jambo muhimu.
-
Waziri wa Usalama wa Taifa nchini Iran: Harakati zote za adui zinafuatiliwa kwa karibu
May 19, 2017 11:53Waziri wa Usalama wa Taifa wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, askari wa usalama wa nchi hii watatoa jibu kwa njama yoyote ya maadui.
-
Uchaguzi; hamasa nyengine ya kihistoria iliyoonyeshwa na wananchi wa Iran
May 19, 2017 10:14Uchaguzi wa 12 wa rais, uchaguzi wa tano wa Mabaraza ya Kiislamu ya Miji na Vijiji na uchaguzi mdogo wa bunge la 10 la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran zilifanyika kuanzia saa mbili asubuhi ya leo Ijumaa katika vituo 63,500 vya upigaji kura nchini kote.
-
Rouhani asema mahudhurio makubwa yataimarisha izza, usalama wa Iran
May 19, 2017 03:15Rais Hassan Rouhani wa Iran ametoa wito kwa wananchi kushiriki kwa wingi katika uchaguzi wa rais unaofanyika hii leo hapa nchini akisisitiza kuwa, mahudhurio makubwa katika zoezi hilo yataimarisha izza na usalama wa Jamhuri ya Kiislamu.
-
Kiongozi Muadhamu awataka wananchi wa Iran wajitokeze kwa wingi katika uchaguzi wa leo
May 19, 2017 00:09Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza juu ya udharura wa wananchi wa Iran kujitokeza kwa wingi katika uchaguzi wa leo.
-
Wananchi wa Iran leo wanashiriki katika uchaguzi wa Urais
May 18, 2017 23:52Wananchi wa Iran waliotimiza masharti ya kupiga kura leo wanaelekea katika masanduku ya kupigia kura kwa ajili ya kumchagua Rais wa nchi.