-
Kingozi Muadhamu aamuru Jeshi la Iran liunde kituo maalumu cha vita dhidi ya Corona
Mar 12, 2020 23:09Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Alhamisi usiku alitoa amri kwa Meja Jenerali Mohammad Baqeri Mkuu wa Kamandi ya Majeshi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kutaka kamandi hiyo iunde 'Kituo cha Afya na Matibabu' kwa lengo la kukabiliana na ugonjwa wa COVID-19 ambao ni maarufu kama virusi vya Corona.
-
Sisitizo la Kiongozi Muadhamu kuhusu udharura wa kuwa macho mbele ya njama za maadui na kuwa tayari kutoa jibu na pigo mkabala
Feb 24, 2020 03:31Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amewashukuru wananchi kwa kuufuzu kwa kiwango cha kuridhisha mtihani mkubwa wa uchaguzi na kuweza kuzima propaganda za kila upande za maadui na kutumia kwao vibaya suala hilo na akasisitiza kwamba: Taifa zima linapaswa kuwa macho na kujiweka tayari kukabiliana na njama za adui zinazolenga kutoa pigo kwa mihimili tofauti ya nchi.
-
Uchaguzi na uwezo unaozidi kuongezeka wa taifa la Iran mkabala wa Marekani kwa mtazamo wa Kiongozi Muadhamu
Feb 19, 2020 04:32Ayatullah Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Jumanne asubuhi alikutana na maelfu ya wananchi kutoka mkoa wa Azerbaijan Mashariki na kusema kushiriki kwenye uchaguzi ni wajibu wa kidini, kitaifa na kimapinduzi na haki ya kiraia ya wananchi wote.
-
Hotuba za Kiongozi Muadhamu Katika Sala ya Ijumaa Tehran; ubainishaji wa nguvu na adhama ya Iran
Jan 18, 2020 04:23Ayatullah Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu katika hotuba zake za Sala ya Ijumaa wiki hii mjini Tehran, alisema: "Kushiriki kimuujiza taifa la Iran katika mazishi ya shahidi mtoharifu Qassem Soleimani na wenzake na pia jibu kali la IRGC lililotolewa kwa kushambulia kituo cha Ainul Assad cha Jeshi la Marekani (nchini Iraq) ni siku mbili ambazo zinaweza kutajwa kuwa Siku za Mwenyezi Mungu (Ayamullah). Siku hizi zimejaa somo na ibra na ni za kuainisha hatima."
-
Jenerali apaa na kukumbatiwa na Malaika
Jan 12, 2020 08:48مِنَ الْمُؤْمِنِینَ رِجَالٌ صَدَقُوا مَا عَاهَدُوا اللَّهَ عَلَیْهِ فَمِنْهُمْ مَنْ قَضَى نَحْبَهُ وَمِنْهُمْ مَنْ یَنْتَظِرُ وَمَا بَدَّلُوا تَبْدِیلًا
-
Sisitizo la Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi kuhusu udharura wa kutekeleza maamuzi ya wakuu wa nchi na ulazima wa kuwa macho mbele ya wanaotaka kuvuruga utulivu na amani katika jamii
Nov 19, 2019 02:25Katika siku za hivi karibuni, baadhi ya miji ya Iran imeshuhudia ukosefu wa usalama kufuatia uamuzi wa viongozi wa mihimili mitatu ya dola kutekeleza mpango wa usimamizi bora wa mafuta ya petroli. Matukio hayo chungu ambayo yaliandamana na ghasia na utumiaji mabavu na hivyo kupelekea kuharibiwa au kuteketezwa baadhi ya maeneo ya umma pia yamepelekea watu kadhaa ya kupoteza maisha.
-
Sisitizo la Kiongozi Muadhamu la kutotosheka na mafanikio ya sasa ya kisayansi nchini Iran
Aug 08, 2019 03:17Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Khamenei Jumatano asubuhi alikutana na vijana kadhaa wasomi bingwa wenye vipaji ambao wamepata medali katika Olimpiadi za kimataifa za sayansi na pia vijana wa timu ya taifa ya voliboli (mpira wa wavu) ya Iran ambao wamefika katika kilele cha mchezo huo duniani. Katika kikao hicho, aliwapongeza vijana hao kutokana na uhodari, umahiri na busara yao na kusistiza kuwa, njia hiyo ya utaalamu bingwa haipaswi kuwa na kikomo.
-
Kiongozi Muadhamu: Tumeanza kupunguza ahadi zetu za JCPOA na tutaendelea kupunguza
Jul 16, 2019 06:52Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amekosoa vikali misimamo ya nchi za Ulaya na kushindwa kwao kutekeleza ahadi zao ndani ya mapatano ya nyuklia ya JCPOA na kusisitiza kwa kusema: Sisi ndio kwanza tumeanza kupunguza hadi zetu ndani ya mapatano hayo na bila ya shaka tutaendelea tu kupunguza utekelezaji wa ahadi zetu ndani ya JCPOA.
-
Jumanne, Juni 4, 2019
Jun 03, 2019 21:46Leo ni Jumanne tarehe 29 Ramadhani 1440 Hijria inayosadifiana na Juni 4 mwaka 2019 Milaadia.
-
Kiongozi: Walanguzi na wahalifu katika mitandao ya kijamii washughulikiwe vikali
Apr 28, 2019 11:47Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema jeshi la polisi lina nafasi muhimu katika kulinda usalama katika Intaneti na mitandao ya kijamii na kuongeza kuwa: "Jeshi la polisi linapaswa kukabiliana vikali na walanguzi wa bidhaa na wahalifu wa intaneti na mitandao ya kijamii."