-
Juhudi za G7 za kukabiliana kiuchumi na China
Jun 28, 2022 21:48Viongozi wa mataifa saba yaliyoendelea kiviwanda, G7, wameafiki kuzindua mpango kabambe wa kuwekeza katika miundo msingi kwenye nchi zinazoendelea. Viongozi hao wametangaza kuwa, nchi za G7 zinakusudia kutenga dola bilioni 600 kwa ajili ya mpango huo ifikapo 2027.
-
China: Kuwepo kijeshi Marekani katika Ghuba ya Taiwan ni tishio kwa amani ya dunia
Jun 25, 2022 21:57Afisa mmoja wa jeshi la China amesema, kuruka ndege za kivita na za ugunduzi za Marekani katika anga ya Ghuba ya Taiwan ni kitendo cha kichochezi na tishio kwa amani ya dunia.
-
Raeisi: Iran ni mshirika endelevu wa BRICS katika nishati
Jun 24, 2022 23:51Rais Ebrahim Raeisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema Iran inaweza kuwa mshirika endelevu wa kuunganisha nchi wanachama wa BRICS katika maeneo muhimu ya kupitisha nishati na masoko makubwa duniani kwa kuzingatia nafasi yake ya kipekee ya jiografia ya kisiasa na jiografia ya kiuchumi.
-
Harakati hatari za Marekani Mashariki mwa Asia
Jun 17, 2022 20:50China imeitaka Marekani ikomeshe harakati zake hatari na za kichochezi eneo la Asia Mashariki ilikiwa ni pamoja na harakati zake za kijasusi.
-
Kamishna wa UN wa Haki za Binadamu aitaka China ipitie upya sera zake dhidi ya ugaidi
May 29, 2022 07:41Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa ameitaka China kupitia upya sera zake za kupambana na ugaidi ili kuhakikisha zinazingatia viwango vya kimataifa vya haki za binadamu.
-
China yawaasa viongozi wa Marekani wachunge kauli zao kuhusiana na Taiwan
May 24, 2022 02:48China imetoa jibu kali dhidi ya uingiliaji wa waziwazi wa Marekani katika masuala ya ndani ya nchi hiyo. Beijing imewaasa viongozi wa Washington wachunge kauli wanazotoa kuhusiana na Taiwan.
-
Safari ya Waziri wa Ulinzi wa China mjini Tehran; ukurasa mpya katika uhusiano wa kiulinzi na kijeshi wa pande mbili
Apr 28, 2022 02:41Jenerali Wei Fenghe, Waziri wa Ulinzi wa China aliwasili mjini Tehran siku ya Jumatano kwa ajili ya kuonana na kufanya mazungumzo na Brigedia Jenerali Mohammad Reza Gharaei Ashtiani, Waziri mwenzake wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Onyo jipya la kijeshi la Marekani kwa China
Apr 24, 2022 21:48Mashindano ya kijeshi na kiusalama baina ya Marekani na China katika eneo la Indo-Pasifiki yamechukua muelekeo mpya kutokana na jitihada za pande mbili za kujiimarisha kijeshi katika eneo hilo muhimu kistratijia.
-
Jumapili tarehe 24 Aprili 2022
Apr 23, 2022 21:52Leo ni Jumapili tarehe 22 Ramadhani 1443 Hijria sawa na Aprili 24 mwaka 2022.
-
China yaonya kuhusu matokeo mabaya kimataifa ya vikwazo dhidi ya Russia
Apr 15, 2022 03:03Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China ameonya dhidi ya kuenea ulimwenguni taathira hasi za vikwazo vya nchi za Magharibi dhidi ya Russia. Zhao Lijian pia ameitaka Marekani kuchukua jukumu maalum la kuzingatia sheria za mfumo wa uchumi wa dunia na kudumisha uthabiti wake.