-
Jeshi la Iraq: Tumekomboa 90% ya mashariki mwa mji wa Mosul kutoka Daesh
Jan 17, 2017 03:38Kamanda mwandamizi wa Kitengo cha Kupambana na Ugaidi cha Jeshi la Iraq (CTS) amesema askari wa nchi hiyo wamefanikiwa kukomboa karibu asilimia 90 ya eneo la mashariki mwa mji wa Mosul kutoka mikononi mwa genge la kigaidi la Daesh.
-
Mkuu wa OSCE: Maelfu ya raia wa nchi za Ulaya wamejiunga na makundi ya kigaidi Iraq na Syria
Jan 14, 2017 09:54Mwenyekiti wa Shirika la Usalama na Ushirikiano wa Ulaya (OSCE) amesema kuwa, karibu raia elfu kumi wa nchi za bara hilo wanashirikiana na kundi la kigaidi la Daesh katika nchi za Syria na Iraq.
-
Majengo kadhaa ya serikali mjini Mosul yakombolewa kikamilifu na jeshi la Iraq
Jan 13, 2017 11:14Jeshi la Iraq kwa kushirikiana na harakati ya kujitolea ya wananchi ya Hashdu sh-Sha'abi limefanikiwa kukomboa majengo ya serikali ikiwemo ofisi ya gavana na makao makuu ya serikali mjini Mosul, mkoani Nainawa (Nineveh)
-
Syria yaapa kulipiza kisasi shambulizi la Israel dhidi ya uwanja wa ndege wa Mezzah
Jan 13, 2017 00:43Jeshi la Syria limetangaza kuwa utawala wa kizayuni wa Israel umeshambulia uwanja wa ndege wa kijeshi wa Mezzah ulioko magharibi mwa mji wa Damascus na kuutahadharisha utawala huo kuhusu taathira mbaya za shambulizi hilo.
-
Wapiganaji zaidi ya 200 wa kundi la kigaidi la Daesh waangamizwa Mosul, Iraq
Jan 10, 2017 01:19Kamanda wa operesheni ya kukomboa mji wa Mosul uliokuwa ngome kuu ya kundi la kigaidi la Daesh nchini Iraq amesema kuwa magaidi wasiopungua 200 wa kundi hilo wameangamizwa katika operesheni iliyofanywa na jeshi la Iraq jana Jumatatu katika mji huo.
-
Magaidi wa Daesh walipua daraja linalounganisha mji wa Mosul
Jan 08, 2017 04:10Kamanda wa operesheni za kuukomboa mkoa wa Nainawa (Nineve) kaskazini mwa Iraq, amesema kuwa, genge la kigaidi na kitakfiri la Daesh, limeripua upande wa kulia wa daraja la Mto Tigris linalouonganisha mji wa Mosul na maeneo mengine.
-
Marekani: Tulianzisha ISIS ili kumpindua Bashar al Assad
Jan 07, 2017 12:34Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani amekiri kuwa lengo lao kuu la kuanzisha genge la kigaidi la Daesh (ISIS) ni kuipindua serikali ya Rais Bashar al Assad wa Syria. Amesema, Washington iliruhusu kuanzishwa kundi la ISIS ili kufanikisha jambo hilo.
-
Magaidi watwangana wenyewe kwa wenyewe Syria
Jan 06, 2017 23:49Mapigano yamezuka baina ya magenge ya kigaidi ya ISIS (Daesh) na Jabhat al Nusra (Fat'h al Sham) katika kambi ya wakimbizi ya Yarmouk, kusini mwa Damascus, mji mkuu wa Syria.
-
Maji yamfika shingoni Abubakar al-Baghdadi, ateua warithi wake
Jan 05, 2017 12:40Kiongozi wa kundi la kigaidi la ISIS (Daesh) Ibrahim al-Samarrai, maarufu kama Abubakr al-Baghdadi ameteua watu watatu ambao wanatazamiwa kuchukua nafasi yake.
-
Magaidi 250 wa Daesh waangamizwa mashariki mwa mji wa Mosul Iraq
Jan 05, 2017 04:23Kamanda wa vikosi vya radiamali ya haraka vya Iraq jana usiku alitangaza habari ya kuangamziwa magaidi wa kundi la kitakfiri la Daesh wasiopungua 250 katika muda wa masaa 24 yaliyopita. Magaidi hao waliuawa katika oparesheni ya kuyakomboa maeneo ya mashariki mwa mji wa Mosul.