-
Kamanda wa jeshi la Ethiopia: Tunaweza kuzima shambulio dhidi ya al Nahdha
Oct 01, 2020 07:04Kamanda wa Jeshi la Anga la Ethiopia amekariri tena kwamba nchi yake ina uwezo wa kuziuia shambulizi lolote dhidi ya bwawa na Renaissance (al-Nahdha) linalojengwa juu ya maji ya Mto Nile ambalo limesababisha mgogoro mkubwa baina ya nchi hiyo na nchi za Misri na Sudan.
-
Watu milioni moja waathiriwa na mafuriko nchini Ethiopia
Oct 01, 2020 04:20Umoja wa Mataifa umeripoti kuwa watu milioni moja wameathiriwa na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa zinazonyesha nchini Ethiopia, ambapo laki tatu miongoni mwao wamelazimika kuyahama makazi yao.
-
Ethiopia imemfungulia mashtaka ya ugaidi Jawar Mohammed na wanaharakati wengine
Sep 19, 2020 22:45Ethiopia imewasilisha mashtaka ya ugaidi dhidi ya Jawar Mohammed kiongozi mkuu wa upinzani nchini humo na wanaharakati wengine; hatua ambayo huwenda ikachochea zaidi machafuko katika eneo la Oromo nchin humo.
-
Ethiopia kuwarejesha nyumbani maelfu ya wahajiri kutoka Saudia kwa kuhofia maisha yao
Sep 18, 2020 06:10Serikali ya Ethiopia imetangaza kuwa itawarejesha nyumbani wahajiri karibu 2,000 kutoka Saudi Arabia katika wiki zijazo, kutokana na wasiwasi mkubwa wa jamii ya kimataifa juu ya hali mbaya inayoshuhudiwa katika kambi za wahamiaji nchini humo.
-
Watu 30 wauawa katika mashambulizi ya wanamgambo nchini Ethiopia
Sep 18, 2020 03:37Watu wasiopungua 30 wameuawa katika mashambulizi ya wanamgambo waliobeba silaha katika eneo la Benishangul-Gumuz, magharibi mwa Ethiopia.
-
Jumamosi, 12 Septemba, 2020
Sep 11, 2020 20:11Leo ni Jumamosi tarehe 23 Mfunguo Nne Muharram 1442 Hijria mwafaka na tarehe 12 Septemba 2020 Miladia.
-
Mkoa wa Tigrey nchini Ethiopia kuendesha uchaguzi; umekaidi agizo la serikali
Sep 04, 2020 22:05Mkoa wa Tigrey wa kaskazini mwa Ethiopia umepanga kuendesha uchaguzi Jumatano ijayo ikiwa ni kukaidi agizo la serikali ya shirikisho ya nchi hiyo.
-
Sudan yataka mzozo wa Bwawa la al-Nahdha ujadiliwe na marais wa nchi husika
Aug 30, 2020 07:29Serikali ya Khartoum imetoa mwito wa kujadiliwa mzozo wa Bwawa la al-Nahdha na marais wa Sudan, Misri na Ethiopia.
-
Mamia ya wahajiri wa Kiethiopia wauawa kwa kupigwa risasi na askari wa Saudia
Aug 13, 2020 22:27Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limeripoti kuwa makumi ya wahajiri wa Kiethiopia waliokimbia vita kaskazini mwa Yemen wameuawa kwa kupigwa risasi na askari wa mpakani wa Saudi Arabia.
-
Ethiopia yaionya Misri kuhusu mpango wake wa kuanzisha kituo cha kijeshi Afrika Mashariki
Aug 13, 2020 09:39Ethiopia imetoa onyo kuhusu uamuzi iliochukua Misri wa kutaka kuanzisha kituo cha kijeshi katika eneo la Afrika Mashariki.