-
Ethiopia na Somalia zakubaliana kushirikiana katika kudumisha amani
Jan 03, 2025 08:33Ethiopia na Somalia zimekubaliana kufanya kazi pamoja katika kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia (AUSSOOM).
-
Watu 71 wafariki dunia baada ya basi la sherehe ya harusi kutumbukia mtoni nchini Ethiopia
Dec 30, 2024 08:51Takriban watu 71 wamepoteza maisha nchini Ethiopia baada ya basi lililokuwa limebeba abiria lililpoacha njia na kutumbukia mtoni. Haya yameelezwa na msemaji wa serikali ya jimbo la Sidama kusini mwa Ethiopia.
-
Watu milioni 7.3 waugua Malaria Ethiopia; 1,157 waaga dunia katika miezi 9
Nov 15, 2024 04:13Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza kuwa, watu zaidi ya milioni 7.3 wamepatwa na ugonjwa wa Malaria nchini Ethiopia huku wagonjwa 1,157 wakiaga dunia kwa ugonjwa huo kuanzia Januari Mosi hadi Oktoba 20 mwaka huu.
-
Iran, Ethiopia zajadili BRICS, uhusiano wao na masuala ya kieneo
Oct 23, 2024 06:54Katika mkutano muhimu wa kidiplomasia, Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian amekutana na Abiy Ahmed, Waziri Mkuu wa Ethiopia, ambapo wamejadili masuala muhimu ya pande mbili na kikanda.
-
Mkataba wa ushirikiano wa Mto Nile waanza kutekelezwa licha ya upinzani wa Misri na Sudan
Oct 13, 2024 23:13Waziri Mkuu wa Ethiopia amesema kuwa Mkataba wa Ushirika wa Bonde la Mto Nile (CFA) ulianza kutekelezwa rasmi jana Jumapili licha ya Misri na Sudan kuendelea kuupinga.
-
Mvua kubwa na maporomoko ya udongo yasababisha vifo vya watu 37 kaskazini mwa Ethiopia
Oct 01, 2024 02:51Karibu watu 37 wamepoteza maisha kutokana na mvua kubwa inayoendelea kunyesha kaskazini mwa Ethiopia, ambapo maporomoko ya ardhi na mafuriko yameharibu maeneo mengi ya ukanda huo.
-
Maporomoko ya ardhi yanatishia watu 400,000 kaskazini mwa Ethiopia
Aug 29, 2024 03:50Mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika eneo la kaskazini la Amhara nchini Ethiopia zimewaweka watu 400,000 katika hatari ya mafuriko na maporomoko ya ardhi.
-
Mafuriko yasababisha maelfu ya watu kuhama makazi yao magharibi mwa Ethiopia
Aug 12, 2024 23:29Takriban watu 16,000 wamelazimika kuhama makazi yao na kuelekea katika maeneo salama kutokana na mafuriko yaliyoathiri maeneo ya magharibi mwa Ethiopia.
-
Mvua kubwa yazidisha mateso ya wakimbizi mashariki mwa Sudan
Jul 27, 2024 03:32Mvua kubwa inayoendelea kunyesha huko mashariki mwa Sudan imezidisha mateso ya watu waliokimbia makazi yao haswa katika miji ya Gedaref, Kassala na Halfa Aj Jadeedah.
-
Ethiopia yaanza siku 3 za maombolezo baada ya maporomoko ya udongo kuua 260
Jul 26, 2024 23:59Bunge la Ethiopia limetangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa kuanzia leo Jumamosi kufuatia maporomoko ya udongo yaliyoua mamia ya watu.